Na David John
BENKI ya Barclays k u s h i r i k i a n a n a taasisi ya
Nkwamira imeanzisha mkakati wa kusaidia vijana ambao wamemaliza elimu ya kidato
cha nne na sita na kushindwa kufanya vizuri katika mitihani yao na kukaa
mitaani bila kujishughulisha.Akizungumza na waandishi wa habari Dar
es Salaam jana Meneja Mawasiliano wa benki hiyo Tunu Kavishe alisema benki yake
imetoa kiasi cha sh. milioni 120 kwa taasisi hiyo kwa lengo la kuwasaidia
vijana hao kwa ajili ya kuwapatia mafunzo mbalimbali ya ujasiriamali.
Kavishe alisema utaratibu wa k uwa p a
t a v i j a n a utafanyika katika mikoa miwili ambayo ni Dar
es Salaam pamoja na Morogoro na vijana wanaotakiwa kwa kuanzia ni
100 kati yao 60 watatoka Dar es Salaam na 40 watatoka Morogoro" M p a n g o h u u
utawashirikisha vijana 60 kwa Mkoa wa Dar es Salaam na wengine 40 watatoka
Morogoro na hiyo itatokana na mitihani mbalimbali ambayo itaendeshwa na wataalamu
wa biashara na fedha kutoka vyuo vikuu vya Tanzania," alisema Kavishe.
Aliongeza kuwa vijana wanaotakiwa ni
kuanzia umri wa miaka 15 hadi 35 ambao watachujwa ili kupatikana washindi
wawili katika mafunzo na kuendelea nao.Kwa u p a n d e wa k e Mkurugenzi wa
Taasisi ya Nkwamira, Noreen Mazalla alisema msaada huo utaweza kuwapatia vijana
fursa ya kujiendeleza na kuondokana na hali ya kuwa tegemezi katika familia
zao.
No comments:
Post a Comment