Kassim Mahege na
Esther Macha
MKULIMA mmoja ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Nkwangu Wilaya ya
Chunya mkoani Mbeya ameuawa kikatili baada ya kupigwa fimbo kichwani kutokana
na ugomvi wa kugombea msichana.Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa jana
kwa vyombo vya habari na kamanda wa polisi mkoani humo, Kamishna Msaidizi wa
Polisi Diwani Athumani, alisema mkulima huyo aliyetambulika kwa jina la Seni
Sandu (20) alifikwa na mauti wakati aliposhambuliwa na mkulima mwenzake, Tolo
Seko (20) ambao wote ni wakazi wa Kijiji cha Nkwangu.
Alisema kuwa, tukio hilo lilitokea
Julai 21, mwaka huu, saa 5 usiku,ambapo Bw.Seko alimshambulia kichwani Bw.Sandu
na kumsababishia kifo ambapo chanzo chake ni wivu wa mapenzi; walikuwa
wakimgombania msichana (16) jina tunalo.
“Mt u h umiwa b a a d a ya kufanya
tukio hili alikimbia lakini kutokana na ushirikiano wa wananchi kijijini hapo
walifanikiwa kumkamata na kumfikisha kwenye vyombo husika, tunashukuru
ushirikiano wa wananchi waliofanya,” alisema Kamanda Diwani.Kama n d a At h uma n i alisema kuwa
mtuhumiwa amekamatwa na taratibu za kumpeleka mahakamani zinaendela ili sheria
ichukuwe mkondo wake.
Hata hivyo, Kamanda
Athuman ametoa wito kwa jamii kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi kwani
ni kinyume cha sheria na kudhibiti hasira zao kwa kuyatatua matatizo ya
kimapenzi kwa njia ya mazungumzo ili kuepusha ma d h a r a y a n a y owe z a
kujitokeza
No comments:
Post a Comment