24 July 2013

WATAKIWA KUAGIZA DAWA ZENYE UBORA



Na John Gagarini, Kibaha
MAOFISA wa Serikali kwenye idara ya mifugo wametakiwa kutumia uzalendo wakati wa kuagiza dawa ili kuepuka kuingizwa dawa zisizo na viwango.Hayo yalisemwa mjini Kibaha na mwakilishi wa kitaifa wa kampuni ya Laprovet ya nchini Ufaransa E p h r a h i m Ma s s a w e alipoongea na waandishi wa habari na kusema kuwa baadhi ya maofisa hao wamekuwa wakiagiza dawa zisizo na viwango.

Massawe alisema kuwa kutokana na kuagizwa dawa zisizo na viwango kumesababisha madhara makubwa kwa mifugo ikiwa ni pamoja na kufa hivyo wafugaji kupata hasara kubwa."Ku f a kwa mi f u g o kunatokana na magonjwa mbalimbali hapa nchini kutokana na baadhi ya dawa kuwa kwenye kiwango cha chini hivyo kushindwa kuzuia au kutibu magonjwa yanayokabili mifugo," alisema Massawe.
Aidha, alisema kuwa tatizo kubwa ni ubadhirifu na kutokuwa na uadilifu kwa maofisa hao hali ambayo inasababisha mifugo mingi kufa kwa kupata matibabu ambayo hayalingani na uwezo dawa hizo toka nje ya nchi."Maofisa hao baadhi yao si waaminifu kwani huagiza dawa ambazo hazina viwango licha ya kuwa dawa nzuri zipo hasa baada ya kuingia soko huria, hivyo wasiangalie maslahi binafsi bali waangalie utu na uzalendo kwa nchi yao," alisema Massawe.
Massawe ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa Waganga Wasaidizi wa Mifugo nchini (TAVEPA) alisema kuwa, endapo maofisa hao watakuwa waadilifu watasaidia kuboresha kipato cha wafugaji.Alibainisha kuwa ili kuhakikisha wafugaji wanajua matumizi sahihi kampuni hiyo inatoa mafunzo pamoja na ushauri wa namna ya ufugaji wa kisasa ili kuongeza tija kwani ufugaji ni mkombozi wa nchi kwani inaliingizia pato kubwa la taifa.

No comments:

Post a Comment