30 July 2013

AKESHA AKISIMAMIA UCHIMBAJI WA KISIMA



 Na Mashaka Mhando, Korogwe
MBUNGE wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Stephen N g o n y a n i ' P r o f e s a Majimarefu' kwa siku tatu mfululizo amekuwa akikesha katika Kijiji cha Magamba Kwalukonge kusimamia uchimbaji wa kisima ili kutatua kero ya maji inayowakabili wananchi wa kijiji hicho.

Mwandishi wa habari hizi, alimshuhudia mbunge huyo akishinda na wananchi wake wakifuatilia uchimbaji wa kisima hicho unaofanywa na Kampuni ya Sum-Hidrogeo Works ya jijini Dar es Salaam.
Hata hivyo, eneo ambalo lilipangwa na wataalamu wa maji kuchimbwa halikuwa lenyewe na hakukuwa na mtu yeyote aliyetajwa kuonesha eneo lisilopangwa ambalo mkandarasi huyo alipochimba na kufika urefu wa mita 120, hakukuwa na maji yaliyotoka.
Mbunge huyo baada ya kuona mkandarasi amechimba umbali huo huku maji yakiwa hayana dalili kupatikana, aliamua kushika chombo kinachopima maji kisha kuyatafuta katika eneo lingine ambalo aliwahamisha wataalamu hao ambao walichimba mita 103 wakapata maji.
"Tunamshukuru mbunge wetu tumepata maji katika kijiji chetu, tulilazimika kulala nje ya nyumba zetu kutafuta maji lakini sasa tunafurahi kupata maji haya," alisema Mwanaisha Lusewa.
Akizungumza mara baada maji kupatikana mbunge huyo alisema kuwa ameweza kutatua kero hiyo ya maji katika kijiji hicho baada ya kupata msaada wa kiasi cha shilingi milioni 20 kutoka kwa kada wa CCM, Mustapha Sabodo kati ya shilingi milioni 41 alizompa.
Alisema amepata msaada wa kuchimbiwa visima viwili katika kijiji hicho na kingine cha Kijango kilichopo Kata ya Magoma msaada ambao utamwezesha kusaidia maendeleo kwa wapiga kura wake.  

No comments:

Post a Comment