Na Mwandishi Wetu
SHULE 100 za sekondari zitanufaika na mradi, Airtel Shule Yetu
utakaowawezesha kupata vitabu vya kiada vitakavyowasaidia katika masomo ili
kuongeza ufaulu.
Kampuni ya
Airtel inayotoa huduma za mawasiliano katika nchi 20 barani Afrika na Asia,
itatumia sh. milioni 150 katika mradi wa Airtel Shule Yetu pamoja na shule 100
zitakazofaidika katika msomo na kuongeza kiwango cha ufaulu nchini
Akizungumza jana
Dar es Salaam, Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando alisema, kwa miaka 11
mfululizo sasa Airtel chini ya mradi wa ‘Shule Yetu’ wameweza kuchangia katika
sekta ya elimu na kuzifikia shule zaidi ya 950 na kutoa vitabu vyenye zaidi ya
thamani ya sh.bilioni 1.6 mpaka sasa.
Alisema kuwa
katika droo maalum iliyoendeshwa na Airtel hivi karibuni shule 100 kutoka
katika mikoa mbalimbali nchini zimechaguliwa na kuingia katika mradi wa shule
yetu kwa mwaka wa 2013 - 2014.
“Tunafahamu jitihada za Serikali chini
ya Wizara ya Elimu katika kupambana na changamoto hizi hivyo tunaungana na
serikali katika kuinua sekta ya elimu kupitia mradi huu wa shule yetu ambao
umeleta tija na kuleta mfanikio katika shule walizoweza kuzifikia.
Tunaahidi kuendelea kuisaidi jamii
kupitia miradi yetu mbalimbali tuliyonayo hususan katika elimu,” alisema.
Awali Kaimu Mkurugenzi ukuzaji
na rasilimali wa Mamlaka ya Elimu (TEA), Bi. Sylivia Gunze alisema kuna
changamoto zinazoikabili sekta ya elimu ikiwemo uhaba wa vitabu shuleni ambapo
kwa sasa uwiano wa vitabu shuleni ni kitabu kimoja kinatumika na wanafunzi 5
hivyo msaada huu utasaidia sana kuongeza kiwango cha ufaulu wa wanafunzi katika
shule zinazofaidika nchini.
No comments:
Post a Comment