15 May 2013

Wanasiasa kufikishwa mahakamani kwa upotoshaji

Na Derick Milton, Simiyu



 MKUU wa Mkoa wa Simiyu, Paschal Mabiti amewataka wanasiasa mkoani humo kuacha mara moja tabia za kuwadanganya au kuwapotosha wananchi kuhusu kilimo cha mkataba hususani zao la pamba.
Alisema, yeyote ambaye ataenda kinyume na agizo hilo atakamatwa ili kufikishwa
mahakamani, sheria ichukue mkondo wake.
Hayo aliyasema jana ofisini kwake mjini Bariadi wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo alikuwa anazungumzia juu ya zao la pamba msimu huu.
Alisema kuwa, katika msimu uliopita wa zao hilo baadhi ya wanasiasa walipita kwa wakulima kuhamasisha wakatae kilimo cha mkataba kwa madai wakijiunga watanyang'anywa mashamba yao na wafanyabiashara.
Mkuu huyo alisema, baada ya wakulima kuambiwa hivyo na wanasiasa hao waliokuwa wame j i u n g a wa l i a n z i s h a mgogoro mkubwa kati yao na wafanyabiashara hadi kusitishwa kwa kilimo hicho.
Kutokana na hali hiyo, Mabiti aliamua kupiga marufuku kwa mwanasiasa yeyote atakayebainika anapinga kilimo cha mkataba kwa msimu ujao kuwa atakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani.
Alibainisha kuwa, hali ya zao la pamba kwa msimu huu ni mbaya katika uzalishaji wake kuwa mdogo, na kutaja sababu kuwa ni kusitishwa kwa kilimo cha mkataba baada ya kuwepo mgongano baina ya wahusika katika kilimo hicho.
Pia alisema, kwa sasa serikali pamoja na wadau wengine wa zao la pamba wakiwemo wafanyabiashara wanafanya utaratibu wa haraka na ambao utakuwa ni mzuri kuhakikisha kilimo hicho kinarudi ili kumkomboa mkulima.
“Katika utaratibu utakaowekwa hivi karibuni, mtu yeyeyote ambaye ni mwanasiasa atakayeonekana na kubainika anapinga kilimo hicho sitamuonea huruma, nitamkamata na kumchukulia hatua za kisheria labda aongelee nje ya mkoa wangu,”alisema Mabiti.
Alibainisha kuwa, wanasiasa hao wamekuwa wakifanya hivyo kwa maslahi yao binafsi na kusababisha wananchi wengi hasa wakulima kubaki maskini na hata bila kutoa msaada wowote kwa watu hao.

No comments:

Post a Comment