15 May 2013

Ole Naiko ateuliwa balozi wa heshima

Na Rehema Mohamed


 KIONGOZI wa muda mr e f u s e r i k a l i n i n a m t a a l a m u a n a y e t a m b u l i k a kitaifa na kimataifa katika masuala ya uwekezaji, Bw. Emmanuel Ole Naiko, ameteuliwa kuwa balozi wa heshima wa Botswana nchini Tanzania, ambapo makao yake yatakuwa jijini Dar es Salaam.
Akitangazwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Bernard Membe, jijini Dar es Salaam, juzi Bw. Naiko, aliishukuru serikali ya Botswana chini ya uongozi wa Rais Ian Khama na Waziri wa Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa, Bw. Phandu T.C Skelemani, kwa kumteua kuwa
mwakilishi wao hapa Tanzania.
"Naamini ni Mwenyezi Mungu aliyewaongoza na
 mimi napenda kuwahakikishia kwamba sitawaangusha. Nitawawakilisha kwa ukamilifu wote ulio ndani ya uwezo wangu," alisema Bw. Naiko.
Bw. Naiko alimshukuru Waziri Membe kwa kukubali kumkabidhi dhamana hiyo kubwa. "Wewe ni ndugu na rafiki yangu wa muda mrefu naamini uliona ni vyema ukanipa heshima hii wewe mwenyewe," alisema.
Alisema Botswana ina vivutio vingi vya uwekezaji kama Tanzania na kuwa Watanzania na jumuiya y a Af r i k a Ma s h a r i k i wanakaribishwa kuwekeza katika nchi hiyo.
"Nadhani wakati umefika Botswana nayo kupata wawekezaji kutoka Tanzania kama wao walivyowekeza Mlimani City," alisema.
Nc h i y a B o t swa n a imepakana na nchi za Afrika ya Kusini, Zimbabwe, Namibia na Zambia. Ina ukubwa wa sq km 58,2000, wakazi milioni 2.
Ni nchi iliyo na amani na utulivu toka uhuru na ina kiwango kidogo sana cha rushwa barani Afrika.
Nchi hiyo imedhamiria kuongoza katika sekta za fedha, madini hasa uranium, shaba na usafirishaji wa almasi na copper na pia kuendeleza uwekezaji katika sekta ya utalii kwani Botswana ina mbuga nyingi za wanyama na hasa Vistoria Falls ambayo iko mpakani na Zimbabwe na Zambia katika mji wa Kasane.
"Watanzania walioko huko wameanzisha chama chao na mimi nilikutana nao nilipokuwa TIC," alisema.
Kodi ya mapato katika nchi hiyo ni asilimia 22; VAT ni asilimia 12 na pia kuna msamaha wa kodi kwa wawekezaji ni kati ya miaka mitano mpaka 10.

No comments:

Post a Comment