15 May 2013

Kukosoana ni kuiimarisha CCM-Jerry Silaa


Na Mwandishi Wetu,
Moshi


 MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmashauri K u u y a Ta i f a , (NEC) wa Chama Cha Mapinduzi, (CCM), Bw. Jerry Silaa, amesema kukosoana miongoni mwa viongozi ndani ya CCM na Serikali ni njia mojawapo ya kukiimarisha chama hicho na isitafsiriwe vingine.
Bw. Silaa ambaye pia ni Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Jijini Dar es Salaam, aliyasema hayo mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro, wakati wa hafla ya kuwapokea wanachama wapya 155 wa CCM wa tawi la CCM la Chuo Kikuu cha Ushirika na Biashara, cha mjini Moshi, (MUCCoBS).
"Ni vyema tukajenga tabia ya kukosoana pale tunapoona
mwenzetu au wenzetu wamepotoka katika kutekeleza ilani ya chama chetu la sivyo ahadi zetu kwa wananchi na malengo ya ilani yetu ya miaka mitano hayatatimia," alisema na kuongeza kuwa makosa anayoyafanya mtu yawe ni ya kwake na kuwajibika nayo na si chama wala serikali.
Bw. S i l a a a l i s ema pia haitakuwa vyema k u w a c h u k u l i a w a l e wanaojitolea kukikosoa chama au serikali kama wasaliti na kwamba kwa kufanya hivyo itakuwa ni sawa na kubariki mabaya ambayo yanakemewa.
"Wanaokosoa mapungufu katika utekelezaji wa ilani yetu wasionekane kuwa ni wasaliti kwa kuwa kwa kufanya hivyo tutakiangamiza chama chetu ambacho bado watu wana imani nacho," alionya.
Alitoa mwito kwa viongozi wa CCM MUCCoBS , kuungana na wale wa Umoja wa Vijana wa CCM, (UVCCM), Mkoa wa Kilimanjaro pamoja na wenzao wa mikoa mingine ili kuangalia uwezekano wa k uwa s i l i s h a k e r o zinazohusiana na mapungufu yaliyoko katika bodi ya mikopo kwa wanafunzi wa taasisi za elimu ya juu na changamoto zake ili kuzitafutia ufumbuzi.
Awali katika risala yake, kaimu katibu wa CCM MUCCoBS, Bw. David Warioba, alisema kuwa moja
 inayowakabili wanafunzi ni mikopo kwa ajili ya wanafunzi hasa wale wa diploma ambao wanataka kuendelea na mafunzo katika ngazi ya shahada.
"Kuna wanafunzi zaidi ya 700 wa ngazi ya diploma hapa MUCCoBS ambao wangependa kuendelea katika ngazi ya shahada, lakini wanashindwa kutokana na serikali kupitia bodi ya mikopo kutoa kipaumbele kwa wale waliotokea kidato cha sita," alisema.
Aidha alitoa wito kwa CCM kupitia Serikali yake kuwachukulia hatua wale wote wanaotumia dhamana waliyopewa kujinufaisha wenyewe jambo ambalo alisema limechangia watu kuinyooshea serikali kidole pamoja na mambo mazuri ambayo imeyafanya na inayoendelea kuyafanya.
Kwa u p a n d e wa k e Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kilimanjaro, Bw. Frederick Mushi, alitoa wito kwa CCM na serikali yake kuwatumia wasomi katika kutekeleza ilani yake.

1 comment:

  1. SI NASIKIA VYAMA HAVITAKIWI KWENYE TAASISI ZA LEARNING HAO CCM SIO CHAMA?

    ReplyDelete