15 May 2013

Katiba Mpya kupingwa mahakamani

Na Goodluck Hongo


 JUKWAA la Katiba nchini, linakusudia kufungua kesi ili kuiomba mahakama isitishe mchakato wa Katiba Mpya hadi Tume ya Mabadiliko ya Katiba na wadau wakubaliane mambo ya msingi ndipo mchakato huo uendelee.
Lengo la jukwaa hilo ni kutafuta haki za Watanzania ili waweze kupata Katiba Mpya waitakayo si vinginevyo.
Mwenyekiti wa jukwaa hilo, Bw. Deus Kibamba aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na
waandishi wa habari akidai mchakato huo una kasoro nyingi.
 Alisema hoja walizoamua kuziweka bayana ni mchakato huo ambao unaendelea kushindwa kurekebisha makosa ya miaka iliyopita katika kuandika Katiba ambayo ni uelewa, hamasa na ushiriki duni wa wananchi katika mchakato wa Katiba yao.
Aliongeza kuwa, jukwaa hilo limeunda timu ya mawakili 10 wakiongozwa na Mwanasheria maarufu wa masuala ya Haki za Binadamu, Dkt. Rugemeleza Nshala.
“Hivi sasa tunaandaa hoja mu h imu z a k u z iwa k i l i s h a mahakamani ndani ya siku saba zijazo, tunawaomba Watanzania watuelewe kuwa tunakwenda mahakamani si kuvuruga mchakato huu bali kuurekebisha.
“Mchakato huu umeshindwa kurekebisha makosa ya miaka ya nyuma hivyo Katiba itakayopatikana inaweza kuwa mbaya zaidi kuliko hii tuliyonayo kwa kuligawa Taifa,” alisema.
Alisema sababu nyingine ya kwenda mahakamani ni juhudi walizozifanya kutaka kuonana na Waziri wa Katiba na Sheria zaidi ya mara moja ili wazungumze naye kuhusu suala hilo pamoja na kumuona Rais Jakaya Kikwete kushindikana.
Bw. Kibamba alisema ahadi alizotoa Rais Kikwete kuhusu mchakato huo hazioneshi dalili ya kutekelezwa kutokana na tume kusuasua katika utekelezwaji wake.
“Awali tume ilipoteuliwa, wananchi walikuwa na imani nayo kutokana na watu waliopewa dhamana hiyo...mwanzo walipewa sh. bilioni nane na mwaka 2012 walitengewa sh. bilioni 34, pesa hizi wanapewa wao lakini bado wanachelewa kutoa rasimu yake.
“Tunaitaka Serikali ifungue ma s i k i o kwa k u t e k e l e z a makubaliano waliyoafikiana na vyama vya siasa...Uchaguzi wa Mabaraza ya Katiba umevurugwa na tume kwa makusudi kwa kushirikiana na Chama Cha Mapinduzi (CCM),” alisema.
Aliongeza kuwa, chama hicho kilitoa fomu za kugombea nafasi hiyo wakati kazi hiyo ni ya tume hivyo ni wazi kuwa mchakato huo ukiendelea, katiba ijayo itakuwa ya CCM si ya Watanzania.
Alisema kwa sasa mchakato huo hauna uongozi na mwelekeo madhubuti kutokana na wananchi wengi walitoa malalamiko ya kuvurugwa kwa uchaguzi wa Wajumbe wa Mabaraza ngazi ya Kata na Wilaya, kutosikilizwa.
Bw. Kibamba alisema baada ya kufungua kesi hiyo, jukwaa hilo halitazungumzia mchakato huo wakisubiri uamuzi wa mahakama

1 comment:

  1. HIVI KWA NINI KATIBA IWE YA VYAMA VYA SIASA TU TATIZO NI MTU MMOJA AWE MAHAKAMA, NDIYE SPIKA NA NDIO RAIS. HAWA WACHUMIA TUMBO WATATUFIKISHA PABAYA. HONGERA JUKWAA LA KATIBA, TUNATAKA NA SISI VIGANJA NA MASHATI TUSHIRIKISHWE KWANI TUNA MIMILI YA DOLA IWAJIBIKE KWA WATU NA HATUTAKI WANAOJIITA WAISLAMU NA WAKIRISTO KUSHIRIKI KATIKA UUNDAJI WA KATIBA YETU WAUNDE KATIBA ZAO ZA KUCHANGISHA SADAKA NA SIO KATIBA YA WATANZANIA

    ReplyDelete