15 May 2013

CCM yamteua Mattar kuwania ubunge Chambani

Na Mwandishi Wetu


 KAMATI Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), imemteua Mattar Sarahan Said, kuwa mgombea wake wa chama hicho katika Jimbo la Chambani, Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba.
Uamuzi huo umefikiwa kwenye kikao cha siku moja kilichofanyika mjini Dodoma jana chini ya Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete.
Pia chama hicho kimewateua Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Balozi Seif Idd na Mwenyekiti mstaafu wa CCM ambaye pia ni Rais mstaafu wa awamu ya pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi, kufunga kampeni hizo.

No comments:

Post a Comment