01 February 2013

Jahazi lazama Z'bar, 10 wahofiwa kufa *22 waokolewa, lilikuwa na abiria 32


Na Mwandishi Wetu

WATU 11 wanahofiwa kufa maji baada ya jahazi la Sunrise, ambalo lilikuwa likitokea mkoani Tanga kwenda Zanzibar kuzama katika eneo la Nungwi.

Habari zilizolifikia gazeti hili ambazo zimethibitishwa na baadhi ya Maofisa wa Jeshi la Polisi Zanzibar, zilidai jahazi hilo lilibeba watu 32 ambapo hadi jana mchana, 21 walikuwa wameokolewa.

Inadaiwa kuwa, jahazi hilo mbali ya kubeba abiria pia lilikuwa na mizigo ambapo jitihada za kuwatafuta abiria wengine zinaendelea na hakuna taarifa za mtu aliyepoteza maisha hadi sasa

kutoka pangani kwenda kwenda zanzibar- abiria 27 na manahodha watano eneo la maziwe, jirani na Nungwi kati yao 21 wameokolewa wakiwa hai 11 hawjulikani walipopigwa
lilikuwa la kusafirisha mizigo kwenda zanzibar

Msemaji Mohamed Muhina msemaji wa Jeshi la Polisi wakati akihojiwa na idhaa ya kiswahili ya BBC alisema manahodha  wameokolewa baadhi yao hawajapatikana





"Ni Kweli taarifa za tukio hilo zipo lakini sina taarifa zaidi, labda unaweza kuwasiliana na Kamanda wa Polisi Kaskazini Unguja, aliyeko eneo la tukio anaweza kukupa taarifa zaidi," alisema mmoja wa maofisa wa polisi Zanzibar.

Juhudi za kumpata kamanda hiyo aliyetwa kwa jina moja la Ahamada hazikuweza kuzaa matunda kutokana na simu yake kutopokelewa muda. Kuzama kwa jahazi hilo na mfululizo wa ajali za baharini ambazo zimekuwa zikitokea katika habari ya Hindi na kusababisha vifo vya watu wengi.

Mwaka jana Meli moja inayomilikiwa na kampuni ya SEAGAL iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam kwenda Zanzibar Tanzania ilizama katika bahari ya Hindi baada ya kukumbwa na dhoruba kali na hatimaye kupinduka.

Kwa mujibu wa jeshi la polisi visiwani Zanzibar meli hiyo iliondoka Dar es Salaam mchana na imepatwa na ajali hiyo huku ndani yake kukiwa na abiria zaidi ya 200.

Kabla ya meli hiyo kuzama, meli nyingine iliyokuwa ikitoka Zanzibar kwenda Pemba ya MV Spice, ilizama kwenye mkondo wa Nungwe na kusababisha vifi vya watu karibu 200.

No comments:

Post a Comment