19 June 2012
Mh. Temba aja sasa kivingine
Na Amina Athumani
MWANAMUZIKI wa kizazi kipya nchini Mh. Temba kesho anatarajia kutoka na wimbo wake wa kwanza wa taarab utakayojulikana kama 'Usisemwe kwani wewe nani'.
Akizungumza Dar es Salaam jana, mtayarishaji wa wimbo huo Haji Ndanda kutoka studio ya HVP iliyopo Kigamboni, alisema wimbo huo wa taarabu ni wa kwanza kuutoa na kwamba ana imani italiteka soko la muziki huo.
Alisema Temba amezoeleka kuimba muziki wa kizazi kipya na kwamba kwa mara ya kwanza ameamua kuja na staili mpya ya taarabu.
Mtayarishaji huyo alisema wimbo huo utaanza kuonekana na kusikika katika vyombo mbalimbali vya habari kesho na kwamba ipo katika video na audio.
Alisema wimbo huo ameamua kumshirikisha msanii mwenzake wa muziki wa kizazi kipya, Z-Anto ili kuongeza vionjo na kwamba ana imani mashabiki wengi wa taarabu wataupokea vizuri hasa kutokana na uhodari wa Temba aliouonesha katika video ya wimbo huo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment