03 February 2012

Watu wa misituni


PERU,
WAPELELEZI wameambiwa waliache kabila linaloishi maisha yao porini kama ya wahadzabe wa Tanzania, walio katika bonde la mto Amazon.


Wito huo huyo umetolewa baada ya kutolewa picha ya wanafamilia kwenye mtandao.

Walipigwa picha mwaka jana na mtafiti wa historia ya binadamu na makabila na habari kutolewa katika mtandao wa Survival International .

Lakini Mariela Huacchillo, wa ofisi ya inayoshughulika na ulinzi wa Maeneo ya asili alionya kutokaribina na watu hao kitu ambacho kinaweza kusababisha kuambukizwa virusi hatari ambazo haviko katika maeneo yao na wenyeji hao wanaweza kukasirika.

 Huacchillo aliwataka watu wanaokwenda kutojaribu kugusana na jamii hiyo ambayo inajaribu kuwa nje ya dunia.

Aliwatakja watu wanakwenda katika eneo hilo kutowaachia chakula, nguo au zawadi nyingine kwa lengo la kwua karibu nao.

Oktoba mwindaji mmoja alijeruhiwa na mshale butu uliofyatuliwa na mmoja wa wawindaji wa kabila hilo.


Tukio kama hilo liliripotiwa mwaka 2010, ambapo kijana mmoja alipigwa mshale na kujeruhiwa.


Taasisi ya Survival International ilielezea kifo kilichotokea mwaka jana cha Nicolas "Shaco" Flores, ambaye alikuwa akiwapelekea chakula na zawadi nyingine kwa miaka 20 watu hao ambaye alipigwa mshale na watu wengine wasiomfahamu.

Tukio hilo halikuthibitishwa.

Kuna kama makundi 15 ya watu wanaishi msituni yasiyofahamiana katika msitu wa Amazon nchini
Peru, kwa mujibu wa taarifa ya serikali.

Kumekuwa na wapelelezi wanakwenda katika maeneo hayo kwa helikopta kwenye miaradi ya mafuta na gesi kwenye misitu hiyo kitu ambacho kinawafanya watu hao wanaoishi mstuni kutawanyika, wanasema wanaharakati.

No comments:

Post a Comment