03 February 2012

Nyani wafungua milango ya gari


 
CAPE TOWN
NYANI wa walioa katika hifadhi ya Cape Point nje ya jiji la Cape Town, Afrika Kusini wamekuwa wakileta usumbukwa watalii ambapo wana uwezo hata wa kufungua milango ya magari.


Gari linaposimama nyani hayo huenda katika milango ambao kama itakuwa imesahalika kuwekwa kizuizi ndani huweza kufungua ili kuangalia kama kuna chakula.

Nyani kama hao pia wamekuwa wakileta usumbufu katika mpaka kati ya Zimbabwe na Zambia ambapo huvamia magari ili kupata chakula.

"Nyani ni tatizo ambalo linatakiwa kushughulikiwa wanaponguza wageni kwa kutaka kupora vitu," Meneja wa Kituo cha forodha cha Zimbabwe katika mpaka wa Chirundu , Tichaona Phiri,  alialiambia gazeti.

"Wakati mwingine hungata au kupiga watu usoni kama watajaribu kuzuia vitu vyao na wanaweza kuwapora mabegi wanawake na hata kufanya uharibifu wakati wakisaka chakula kwa gari."

Wakati mwingine hupafua magunia ya mahindi kwenye malori yanayopita kwenye mpaka, Kamati ya bunge iliambia baada ya kutembelea hifadhi.

"Nyani hawa wanaweza kunusa harufu ya mahindi kwenye na kufikiri kuwa kuna kiasi kikubwa, ni ngumu sana kuwadhibiti," gazeti lilimkariri Phiri akisema.

"Lakini tatizo ni kwamba wamekwua na tabia kama binadamu na wamekuwa na mbinu,"  alisema Phiri.

No comments:

Post a Comment