*Ni kutokana na mauaji ya wananchi watano Tarime
*Yalaani, yasema huo ni ukiukwaji wa haki za binadamu
Na Agnes Mwaijega
BARAZA Kuu la Chama cha Wananchi (CUF) limemtaka Waziri wa Mambo ya Ndani kuwajibika kutokana na mauaji yaliyotokea wilayani Tarime
lakini pia kufanyika kwa uchunguzi wa kina juu ya tukio hilo.
Hatua hiyo ilifikiwa Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mapendekezo mbalimbali yaliyoazimiwa na kikao cha baraza hilo.
Alisema kuwa baraza hilo linalaani vitendo vya ukiukaji na uvunjaji wa haki za binadamu hususan mauaji ya raia yanayofanywa na Jeshi la Polisi ambayo yamekuwa yakiripotiwa kila mara.
"Inatuumiza sana kwa kuwa inaonekana jambo hili ni la kawaida kwa sababu watendaji wake hawachukuliwi hatua yoyote," alisema.
Prof. Lipumba alisema kuwa baraza hilo pia linamtaka Rais Jakaya Kikwete kutambua kuwa jukumu la kuleta maendeleo ya Watanzania ni la watu wote hivyo serikali yake isisite kutumia sera mbadala za CUF kwa maendeleo ya taifa.
Alisema serikali kupitia wizara ya Fedha na Uchumi na Wizara ya Nishati na Madini inatakiwa kuchukua hatua za kuhakikisha nchi na wananchi wake wananufaika na rasilimali za madini zilizopo hapa nchini hususani madini ya dhahabu ambayo bei yake katika soko la dunia imepanda.
"Dhahabu inayouzwa nje ni dola bilioni 1.5 kwa mwaka sawa na asilimia 40 ya bidhaa za Tanzania zinazouzwa nje ya nchi," alisema.
Alisisitiza kuwa baraza hilo linataka kuona utajiri wa nchi unawanufaisha wananchi na kuisaidia nchi kujikomboa kutoka katika dimbwi la umasikini na kuacha kutegemea misaada kutoka nje ambayo imeifanya nchi kuwa tegemezi kwa miaka mingi.
Aliongeza kuwa baraza hilo linamtaka Waziri wa Nishati na Madini Bw.William Ngeleja kujiuzulu kwa kuwa ameshindwa kutumia vyanzo vya umeme vilivyopo nchini ili kukabiliana na tatizo sugu la nishati linaloikumba nchi yetu kwa sasa.
Alisema nchi imejaliwa vyanzo vingi ya umeme na maeneo mengi ya maporomoko ya maji,makaa ya mawe ,madini na hata umeme wa jua ambao hauna gharama kubwa ya kufua.
"Ni miaka 50 tangu tupate uhuru hatuna sababu yoyote ya kutokuwa na umeme wa uhakika, ni ufisadi tu ambao umekithiri katika serikali yetu," alisema.
Alisisitiza kuwa serikali ni lazima itambue kuwa hali ya kutokuwa na umeme wa uhakika imezorotesha uzalishaji viwanda,biashara,huduma katika hospitali na shule hivyo kusababisha uchumi wa nchi kuzorota.
Aliitaka serikali kuzingatia mapendekezo na hoja zinazotolewa na kamati ya Nishati na Madini ya Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania zinazolenga kupata ufumbuzi wa matatizo ya umeme.
Pia alisema baraza hilo linaitaka serikali kuwa makini katika suala zima la utunzaji na uhifadhi wa silaha nzito za kivita zenye madhara makubwa na kutaka zihifadhiwe mbali na makazi ya watu ili matukio ya milipuko ya mabomu ambayo yameshatokea mara mbili yasijirudie tena.
CUF NYIE MSILALAMIKE KWANI NYIE PIA KULE ZNZ MPO KWENYE SERIKALI YA ccm WAACHIENI CHADEMA WASEME KWANI WAO NDIO WAPINZANI PEKEE WALIOBAKI NCHI HII
ReplyDeleteMAENDELEO NI KWA WATANZANIA TUKISEMA KWA UMOJA WETU INALETA MAANA ZAIDI KULIKO KUWAACHIA KAZI YA KUSEMA WATU FULANI TU SIJUWI KWA MTAZAMO WAKO UNA MAANA GANI ? KWAMBA MWENZETU UMERIDHIKA SANA MPAKA UWACHE WATU WAKUSEMEE ! MWISHO UTASHINDWA HATA KUMEZA CHAKULA KWA KUDHANI MTU FULANI ATAKUFANYIA HILO
ReplyDeleteMini nafikiri kuwa ni wakati muafaka sasa Raisi wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na serikali yake na chama chake kujiuliza kwa nini Jeshi la polisi badala ya kulinda usalama/uhai wa Mtanzania lenyewe ndilo linaua. Haya tuseme kuwa yamekuwepo maandamano yasiyo halali, mfano Zanzibar wakati wa Mkapa Polisi waliuawa wafuasi wa CUF 25, chama hicho kilifitiniwa kuwa ni chama cha kidini (kiislam). Haya awamu ya Kikwete Polisi wameuawa watu 3 huko Arusha wwafuasi wa CHADEMA, chama hiki nacho kinafitiniwa sasa kuwa ni cha kidini (kikristu). Huko Mara nako Polisi wamewauwa Watu migodini, Kina Zombe nao waliwaua wafanya biashara. Waziri anpotakiwa kujiuzulu si kwamba yeye ndiye aliyeua moja kwa moja. Anahusika kwa kuwa chini ya utawala/uongozi wake yametokea, ajiuzuli ili kuwajibika.
ReplyDelete