Na
Elizabeth Mayemba
Uongozi
wa klabu ya Simba umesema kuwa usajili wake katika kipindi hiki cha dirisha
dogo watafanya kimyakimya kwa ajili ya kukwepa hujuma, kwani kuna klabu
zinasubiri klabu hiyo itangaze nia ya kusajili mchezaji fulani ili wavuruge.
Akizungumza na gazeti hili jana mmoja wa wajumbe wa kamati ya usajili
ya klabu ya Simba ambaye hakutaka kuandikwa jina lake gazetini,
alisema watamtangaza mchezaji pale tu watakapoingia naye mkataba.
"Sisi hatusajili kwa kutangaza nia, tutakapomhitaji mchezaji
fulani tutakubaliana naye na kuingia naye mkataba ndipo tutakapomtangaza rasmi
katika vyombo vya habari," alisema Mjumbe huyo.
Alisema kuna klabu zinasubiri kuona Simba inamnyatia mchezaji gani ili
nao waingilie kati, lakini kwa staili hiyo safari hii hawawapati na badala yake
watasikia tu washamsainisha mchezaji wanayemtaka.
Mjumbe huyo alisema timu yao
inamapungufu katika kila idara, hivyo watatafuta wachezaji ambao wataondoa
tatizo hilo kwa lengo la timu yao kutwaa ubingwa msimu huu tofauti na watu
wanavyofikiria.
Alisema kuwa inashangaza kuona baadhi ya
watendaji ndani ya Simba wanathubutu kusema kuwa Simba haichukui ubingwa, hali
ambayo inaonesha ni kuwakatisha wachezaji tamaa na wakati nafasi waliyonayo
wana nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa huo.
Kiongozi huyo alisema kwa sasa mengi
yatasemwa kuhusu timu yao,
lakini wao wanaamini kwamba ubingwa watauchukua na wale wanaotamba mapema kabla
ya mzunguko wa pili haujaanza wataishia kuumbuka.
Simba
wamemaliza ligi hiyo wakiwa na pointi 24 na kushika nafasi ya nne, huku vinara
wa ligi hiyo wakiwa Yanga wenye pointi 28 ikifuatia Azam FC wenye pointi 27
sawa na Mbeya City
No comments:
Post a Comment