Na Rose Itono
Mhariri na Msanifu Mkuu
Msaidizi wa gazeti la Uhuru, Dunia Mzobora, amefariki dunia usiku wa kuamkia
jana katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kutokana na ugonjwa wa
shinikizo la damu.
Akizungumza na Majira kwa njia ya simu jana, Mhariri
Mtendaji wa gazeti la Uhuru, Josia Mufungo, alisema marehemu kabla ya mauti
yake alikuwa kazini kama kawaida ambapo saa
mbili usiku alimaliza kazi zake na kurejea nyumbani.
Alisema usiku wa saa sita walipata taarifa kutoka kwa
familia yake kuwa Dunia amezidiwa na kukimbizwa haraka hospitali kwa ajili ya
matibabu.
"Marehemu alikimbizwa Hospitali ya Agha Khan lakini
walishindwa na kuamua kumpeleka Muhimbili kwa matibabu zaidi na saa 12 za
asubuhi alifariki", alisema.
Mufungo alisema marehemu alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa
shinikizo la damu kwa muda mrefu na kuongeza kuwa msiba wake utafanyika
nyumbani kwake Tabata Kimanga, ambapo anatarajiwa kuzikwa leo saa 7.00 za
mchana na shughuli zote za mazishi zitakuwa hapo hapo nyumbani kwake.
Alisema marehemu ameacha mjane na watoto watano. Alijiunga na
gazeti la Uhuru mwaka 1989 kama mwandishi
mwanafunzi ambapo baadaye alipanda hadi kufikia nafasi aliyokuwepo
No comments:
Post a Comment