06 November 2013

MBEYA CITY: HATUIHOFI I AZAM FC



Na Ester Maongezi
  Klabu yenye ushindani kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara ya Mbeya City imesema haiiogopi Azam FC na kwamba ipo tayari kuvaana nayo hapo kesho.

  Timu hizo ambazo zina pointi 26 zote isipokuwa Azam inaongoza kutokana na kuwa na wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa,zinatarajiwa kumenyana kesho katika Uwanja wa Chamazi Complex nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
  Akizungumza na mwandishi wa habari hii kwa simu jana Msemaji wa Klabu ya Mbeya City, Fred Jackson alisema wapo tayari kucheza na Azam na hawaiofi i hata kidogo.Jackson alisema hawaigopi Azam, ila wanaipa uzito kama walivyofanya katika timu walizowahi kukutana nazo katika ligi.
 “Hatuiogopi Azam ila tunaipa uzito kama moja ya timu nzuri, ambazo tunakutana nazo katika mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara mwaka huu, ila sisi kama Mbeya City tumejiandaa vya kutosha,” alisema Jackson.
  Jackson aliongeza kuwa wanakiamini kikosi chao kutokana na kwamba hawana majeruhi hata mmoja. Mbeya City inatarajia kuingia jijini Dar es Salaam leo wakitokea Mbeya tayari kabisa kwa ajili kuivaa Azam kesho.

No comments:

Post a Comment