AWASILISHA VIELELEZO KWA WASULUHISHI WA MGOGORO
Na
Penina Malundo
Rais Jakaya Kikwete, amewasilisha utetezi wa Tanzania
kwa jopo la Marais wastaafu wanaotafuta ufumbuzi wa mpaka wa Ziwa Nyasa, kati
ya Tanzania na Malawi.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Bernard Membe,
aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Alisema
utetezi huo uliwasilishwa kwa Rais mstaafu wa Msumbiji Joaquim Chissano ambaye
ndiye Mwenyekiti wa jopo hilo na Rais mstaafu wa Botswana, Bw. Festus Mogae.
Awali,
viongozi hao wastaafu walifanya mkutano kama huo Blantyre, nchini Malawi ambapo
juzi walisikiliza hoja za upande wa pili juu ya mgogoro huo.
"Katika
mkutano huu, Rais Kikwete alitoa maelezo mazuri pamoja na vielelezo
mbalimbali... utetezi wetu ulikuwa wa kisayansi hivyo hatuna hofu yoyote juu ya
hili," alisema.
Bw.
Membe alisema, leo anatarajia kwenda Maputo, nchini Msumbiji, kuwasilisha
maelezo yaliyotolewa na Rais Kikwete mbele ya marais hao wastaafu.
Aliongeza
kuwa, jopo la Wanasheria wa kimataifa bado linaendelea na kazi ya kufanya
utafiti juu ya mgogoro huo kwani jambo hilo kwa kuliangalia ni dogo lakini ni
kubwa.
Alisema kuwa mgogoro huu unaweza kuwa na tambo mbalimbali
kati ya nchi moja na nyingine ingawa tambo hizo zinaweza kuleta athari kubwa
kwa nchi hizo hivyo utafiti zaidi unahitajika.
No comments:
Post a Comment