- ALIKUWA KWENYE MATIBABU AFRIKA KUSINI
- NCCR- MAGEUZI KUZUNGUMZIA MSIBA LEO
Aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba, Dkt. Sengondo Mvungi, amefariki dunia jana alasiri nchini
Afrika Kusini, katika Hospitali ya Milpark, Johannesburg.
Dkt.
Mvungi ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha NCCR-Mageuzi na
Mhadhiri Mwandamizi wa Sheria Chuo Kikuu cha Bagamoyo (UB), alipelekwa nchini
humo baada ya kuvamiwa na kujeruhiwa usiku wa kuamkia Novemba 3 mwwaka huu
akiwa nyumbani kwake, Kimbamba Msakuzi.
Chama
cha NCCR-Mageuzi, kimethibitisha juu ya kifo hicho na kuongeza kuwa, taarifa
kamili zitatolewa leo Makao Makuu ya chama yaliyopo Ilala, kuanzia saa tatu
asubuhi.
Mtoa
habari hizo ndani ya chama ambaye hakutaka jina lake liandikwe
gazetini, alisema marehemu Dkt. Mvungi alikuwa kiongozi mkubwa ndani ya chama na
ametumia fursa hiyo kukifanya chama hicho kiwe na wanachama wengi.
Dkt.
Mvungi baada ya kujeruhiwa kwa mapanga, alikimbizwa katika Hospitali ya Rufaa
Tumbi, iliyopo Kibaha, mkoani Pwani na baadaye kuhamishiwa katika Hospitali ya
Taifa Muhimbili, Kitengo cha Wagonjwa Wanaohitaji Uangalizi Maalumu (ICU).
Kutokana
na hali yake kutoimarika vizuri akiwa hospitalini hapo, Novemba 7 mwaka huu,
Dkt. Mvungi alisafirishwa kwa ndege ya kukodi ya Shirika la Ndege la
Flightlink, kwenda Afrika Kusini kwa matibabu zaidi hadi mauti yalipomkuta
wakati madaktari wakiendelea kuokoa maisha yake.
Msemaji wa Kitengo
cha Taasisi ya Mifupa (MOI), Bw. Jumaa Almas, alisema walilazimika kumsafirisha
Dkt. Mvungi kutokana na afya yake kutoimarika vizuri.
Dkt. Mvungi alipata
majeraha makubwa kichwani ambapio katika msafara wake, aliongozana na Daktari
Bingwa wa Upasuaji Ubongo na Mishipa ya Fahamu Dkt. Clement Mugisha na Muuguzi,
Bi. Juliana Moshi.
Juzi Jeshi la Polisi
nchini kupitia Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Emmanuel Nchimbi, alisema
watu tisa ambao walihusika kumpiga, kumjeruhi na kuiba vitu mbalimbali vya
marehemu Dkt. Mvungi, tayari wamekamatwa.
Dkt. Nchimbi alisema
watu hao walikamatwa katika maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam kwa nyakati tofauti ambapo
awali walikamatwa sita na juzi kufikia tisa.
Kamanda wa Polisi
Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova, ambaye alikuwepo katika
mkutano huo, aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Msigwa Mpopela (30), Shabago
Magozi na Hamadi Ally, jina maarufu 'Hatibu'.
Wengine ni Zakaria
Raphael (dereva wa bodaboda), Mmanda Saluwa, Juma Hamisi, Longisho Semeriko
(muuza ugolo), Paul Jeirosi na mwingine aliyemtaja kwa jina moja la
Kilimimazoka, ambao wote ni wakazi wa Dar es Salaam
"Watuhumiwa hawa
walikutwa na mapanga, kigoda ambavyo vimethibitika kuwa vilitumika katika tukio
hilo, pia walikutwa na simu ya mkononi mali ya Dkt.
Mvungi," alisema.
Kamishna Kova
alisema, katika mahojiano ya awali na watuhumiwa, walikiri kuhusika na tukio hilo na ushahidi
umekamilika kwa asilimia 80.
"Watuhumiwa wote
wamekiri kosa hivyo tunakamilisha upelelezi ili wafikishwe mahakamani mara
moja," alisema.
Marehemu
Dkt. Mvungi, aliwahi kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka
2005 kwa tiketi ya Chama cha NCCR-Mageuzi
What a loss in the academia. Rest in peace beloved
ReplyDeleteI remember him and Dr. Tenga during a research work in Manyara and Arusha regions on pastoralism and policy discourses
ReplyDeleteYour legacy is irrefutable in the academia!