- NI MKENYA ALIYEDAIWA KUMTEKA,KUMTESA
- ASIMULIA MKASA,MWANDISHI AMLIPIA FAINI
Na Rehema Mohamed
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemlipisha
faini ya sh. 1,000 raia wa Kenya,
Bw. Joshua Mulundi baada ya kumtia hatiani katika kesi iliyokuwa ikimkabiliBw. Mulundi
alikuwa akikabiliwa na kesi ya kuidanganya polisi kuwa alihusika katika tukio
la kumteka Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dkt. Steven Ulimboka.
Shauri hilo lililetwa mahakamani hapo mbele ya Hakimu Aloyce
Katemana, kwa ajili ya mshtakiwa huyo kusomewa maelezo ya awali na upande wa
mashtaka ambapo Bw. Mulundi, alikiri kutenda kosa hilo.Hakimu Katemana
aliieleza Mahakama hiyo kuwa, baada ya mshtakiwa kukiri maelezo yote ya kosa,
inamtia hatiani na kumsomea hukumu pamoja na adhabu ya kulipa sh. 1,000 au
kifungo cha miezi sita gerezani.
Akisoma hukumu
hiyo, Hakimu Katemana alisema hukumu hiyo imezingatia maelezo ya upande wa
mashtaka na mshtakiwa alipokuwa akiililia mahakama, hivyo kumpa adhabu ya
kulipa faini au kwenda gerezani miezi sita.
Hata hivyo,
Hakimu Katemana alipomuuliza mshtakiwa kama ana kiasi hicho cha fedha alijibu
hana ambapo mwandishi wa habari wa Kituo cha Radio Times FM, Chipangula Nandule
alijitolea kumlipia faini hiyo.Kabla ya
kutolewa adhabu hiyo, Bw. Mulundi alidai mahakamani hapo kuwa, alikuja Tanzania
kufanya biashara ya nguo ambayo aliunganishwa na kijana mmoja wa mjini Arusha
ambapo akiwa huko, Juni 27, 2012 alitekwa na mtu asiyemjua.
Alisema mtu
huyo alikuwa na silaha, kumpeleka asikokujua na kumlazimisha aende kwenye
Kanisa la Ufufufo na Uzima la Mchungaji Gwajima lililopo Kawe, Dar es Salaam
akasema alichomueleza ambacho ni kumteka Dkt. Ulimboka. Alidai alilazimika
kukubaliana na amri hiyo kutokana na vitisho alivyokuwa akipewa na baada ya
hapo, alipelekwa Kituo cha Polisi Oysterbay na kusisitizwa azungumze
alichokisema na kuahidiwa atapelekwa kwao nchini Kenya na kubadilishiwa maisha
yake.
Huku
akibugujikwa na machozi, Bw. Mulundi alidai “Nikiwa Polisi Central, polisi
mkubwa aliniambia niseme vilevile nilivyoambiwa niseme na walinirekodi,
nilishangaa kuletwa mahakamani nikidaiwa kutaka kumuua Dkt. Ulimboka.
“Sipingani na upande wa mashtaka,
nilivyoletwa nilidhani nimeonewa, nimejifunza kuwa mahakama ni kitu tofauti
sana, siilaumu Serikali, polisi wala upande wa mashtaka maana hata
nisingekubaliana na walioniteka, mimi si bora zaidi ya watu wengine,” aliongeza
mshtakiwa huyo.Alisema kuwa, tukio la kutekwa Dkt.
Ulimboka lilileta shida nchini lakini taarifa alitoa kwa hiari yake kutokana na
vitisho alivyokuwa akivipata ili kuokoa maisha yake.
“Mheshimiwa hakimu, nimekosa mbele ya
Mungu na mahakama ya Tanzania, ningeomba kwa ubinadamu na upendo pia, nimekaa
jela muda mrefu, naomba nipewe adhabu iwe fundisho kwa wengine lakini
nipunguziwe adhabu,” alidai.Bw. Mulundi alidai yeye ni kijana wa
miaka 23, mama yake ni mjane hivyo yupo mwenyewe nyumbani kwao hivyo hakimu
akiwa kama mazazi, amuonee huruma kwani hajui kitakachofanyika kesho.
Awali akisomewa maelezo hayo ya awali
na wakili wa Serikali Tumaini Kweka, alidai mshtakiwa huyo alikuja nchini
akipitia mpaka wa Namanga, Arusha-Dar es Salaam na kwenda kanisani hapo.Alidai mshtakiwa huyo alionana na
Mchungaji Joseph Kiriba na kumweleza kuwa yeye ni miongoni mwa watu waliomteka
na kumtesa Dkt. Ulimboka, kumtupa Mabwepande na taarifa kufika polisi.
Aliongeza kuwa, baadaye mshtakiwa huyo
alipelekwa kwa mlinzi wa amani ambapo alikanusha taarifa za kumteka Dkt.
Ulimboka.
Alidai baada ya polisi kufanyia uchunguzi taarifa hizo,
ilibaini ni kweli hakuhusika hivyo kumbadilishia mashtaka kutoka lile la
kumteka na kumjeruhi, Dkt Ulimboka hadi shtaka la kutoa taarifa za uongo kwa
polisi na kushtakiwa upya
No comments:
Post a Comment