29 October 2013

ALIYEMPIGA MTAWA JELA MIEZI SITA



  Mahakama ya Wilaya ya Musoma, mkoani Mara, imemhukumu mfanyabiashara maarufu mjini humo, Bw. Dola Jamal, kifungo cha miezi sita gerezani kwa kosa la kumshambulia Mtawa wa Kanisa la Katoliki, anaripoti Raphael Okello, Musoma

  Mbele ya Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Faisal Kahamba ilidaiwa na Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Jonas Kaijage kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Juni 10, 2010.
  Alisema siku ya tukio, mshtakiwa alimshambulia kwa vipigo na matusi Mtawa huyo (jina linahifadhiwa) na kusababisha uvunjifu wa amani kwenye jamii.
  Baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo, Hakimu Kahamba alitoa adhabu ya kifungo cha miezi sita jela na kutozwa faini ya sh. 500,000 ili iwe fundisho kwa watu wengine.
  Wakati huo huo, mahakama hiyo juzi ilimhukumu kifungo cha maisha mkazi wa Nyakanga, wilayani Butiama, Nyamhanga Magesa (35) kwa kosa la kuchoma nyumba tatu za mama yake mzazi, Nyangi Waryoba.
  Mbele ya Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Musoma, Emmanuel Ngigwana, ilidaiwa na Mwendesha Mashtata wa Polisi, Theofil Mazuge kuwa, mshtakiwa alivunja kifungu namba 319(a) cha kanuni ya adhabu sura ya 16.
  

No comments:

Post a Comment