Na
Mwandishi Wetu
NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya
Ufundi, Philipo Mulugo, amewataka wazazi, walezi na jamii kwa ujumla kutumia
teknolojia ya elimu masafa na mitandao kwa kupata taarifa za uhakika za
kitaaluma na kimaendeleo.
Akizungumza
wakati wa uzinduzi wa maonesho ya Vodacom Elimu Expo 2013 juzi, jijini Dar es
Salaam, Waziri Mulugo alisisitiza kuwa ushiriki wa wandau wote kuendeleza sekta
ya elimu unafungua fursa ya kupata na kutoa elimu bora kwa kila Mtanzania.
Maonesho
ya Vodacom Elimu Expo 2013 ni ya kwanza nchini Tanzania ambapo yamedhaminiwa na
kampuni ya simu ya Vodacom kupitia huduma yake ya M-Pesa.Waziri
Mulungo alisema: "Hii ni fursa kubwa kwa wote wanaoshiriki maonesho haya
hususan wanafunzi, walimu na wazazi.
Yanatoa
nafasi kwa kila mdau wa elimu kuchangia maendeleo ya elimu nchini."Alisisitiza
kuwa Serikali kupitia wizara ya elimu, ipo katika hatua za mwisho za
kutengeneza mkongo wa taifa utakaounganisha upatikanaji wa mtandao nchi nzima
kapitia programu ijulikanayo kama 'Tanzania
Beyond Tomorrow' kwa kushirikiana na kampuni za mawasiliano katika kuboresha
elimu ya masafa.
"Naipongeza kampuni ya Vodacom kwa kuwa kampuni ya kwanza nchini
kushirikiana na Serikali kutekeleza mpango ili kuhakikisha kuwa sekta ya elimu
inaendelea na kuwa bora zaidi," alisema.Naye Robert
Mihalo, ambaye ni mwanafunzi wa shule ya Green Acres ya jijini alipongeza
wadhamini na waandaaji wa maonesho hayo akisema:
"Nimeweza
kubandilishana mawazo na wanafunzi wa shule zingine. Zaidi ya yote, nimepata
mbinu mpya kwa kupanua wigo wa ushiriki wa wanafunzi katika kuleta elimu bora Tanzania."Naye
Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa Vodacom, Kelvin Twissa, ambao ni
wadhamini wakuu wa maonesho hayo alionyesha matumaini yake kwa maonesho hayo na
kusema kampuni yake inaelewa umuhimu wa elimu kwa kila mtoto kwa hiyo
wanajisikia fahari kudhamini maonesho hayo kwani yanalenga kuboresha elimu ya
Tanzania. Maonesho hayo yamemalizika jana.
No comments:
Post a Comment