Na Rachel
Balama
SHIRIKA l a Viwa n g o nchini
limewatahadharisha waingizaji wa bidhaa kutoka nje ya nchi kwamba bidhaa
watakazoingiza wahakikishe kwamba zimekidhi viwango vinginevyo zitarudishwa
zilikotoka.Kauli hiyo
ilitolewa Dar es Salaam mwishoni mwa wiki na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TBS,
Joseph Masikitiko, wakati alipokuwa akikabidhi leseni na vyeti vya ubora kwa
wazalishaji mbalimbali baada ya kukamilika kwa taratibu za udhibiti ubora.
"Mwito
wangu ni kwamba waingizaji wote wa bidhaa kutoka nje ya nchi wanatakiwa
kuhakikisha bidhaa hizo zimekidhi viwango, tofauti na hapo watatozwa faini na
kisha bidhaa hizo zitarudishwa nje ya nchi," alisema.Alisema mpango
wa kukagua bidhaa za nje ya nchi kabla ya kuletwa nchini unaendelea kuimarika,
wakati TBS ikiendelea kuhakikisha bidhaa za ndani zinakidhi viwango.
Alisisitiza kuwa waagizaji wa bidhaa toka nje ya nchi wanawajibika kuhakikisha
bidhaa wanazoleta nchini zina ubora unaostahili.
Alisema mbali
na kuwa na ubora unaostahili pia bidhaa hizo ziwe zimekaguliwa na kupewa vyeti
vya ubora yaani vinavyotolewa na mawakala walioidhinishwa na shirika hilo.Alisema
utaratibu wa kutoa adhabu utaendelea kwa wale wote wanaokiuka utaratibu huo
ambapo kwa upande wa wakaguzi wa nje ambao hutoa vyeti bila kukagua bidhaa
wakibainika mikataba itafutwa ili kuifanya Tanzania kuwa soko la bidhaa bora.
Masikitiko, aliongeza kuwa shirika
linaendelea kusisitiza kwamba wazalishaji wote wa bidhaa ambazo viwango vyake
ni vya lazima, vikiwemo vyakula kujitokeza kwa hiari kuthibitisha ubora wa
bidhaa zao badala ya kusubiri shuruti inayoendana na kufungwa kwa viwanda vyao.
P i a a l i t o a mwi t o kwa
wajasiriamali wadogo kutumia fursa ya elimu itolewayo na shirika kwa namna
mbalimbali kwani moja ya majukumu ya TBS ni kuwafundisha wazalishaji kuhusu
njia bora za usindikaji na kufikia viwango.Shirika hilo lilitoa jumla ya leseni na vyeti vya ubora 43 kwa bidhaa
mbalimbali baada ya kukamilika kwa taratibu za kukidhi viwango vya TBS.
No comments:
Post a Comment