Na Cornary Anthony, Dodoma
BODI zote na taasisi za mazao nchini
zimetakiwa kuyapatia ufumbuzi matatizo yanayowakabili wakulima katika maeneo
husika na sio kujihusisha zaidi na mazao ya biashara.Hayo yalisemwa na Waziri wa Kilimo
Chakula na Ushirika, Christopher Chiza, wakati akifungua Mkutano wa wadau wa
korosho mkoani Dodoma
juzi.
Chiza alisema kuwa jukumu la kila bodi
la zao la korosho ni kutatua changamoto zote zinazokabili zao hilo kuanzia kwenye kilimo mpaka kwenye soko.
“Haifurahishwi kumuona mkulima ana mazao ya kudumu lakini hayaleti tija kwa
mkulima,”alisema ChizaAlisema wameona katika Mikoa ya Mbeya,
Kagera na Kilimanjaro wana mazao ya kudumu ya migomba lakini uchumi wake
umeimarika sio kama zao la korosho kwani haliko kama
zao la migomba.
Hata hivyo, alisema kuwa anaziomba bodi
zote za mazao nchini yaani mazao ya korosho, pamba, kahawa na Tumbaku zifuate
njia za mkato ya kuweza kutatua matatizo ya wananchi na si vinginevyo.Aidha aliwataka wanunuzi wa korosho
nchini wasipende kuwatumia wawakilishi maana kila wanapohitaji taarifa zozote
wanasema wao sio wazungumzaji. Aliipongeza Bodi ya Korosho Tanzania kwa
kuweza kuongeza wataalamu katika mikoa na Wilaya ambapo hapo awali zilitokea
Wilaya 34 hadi sasa zimefika 42 kwamba huo ni mwanzo.
Kwa u p a n d e wa k e Mwenyekiti wa
Bodi ya Korosho Tanzania,
Anna Abdallah, aliiomba Serikali kuunga mkono Bodi ya Korosho kwa mkakati wake
wa kuwaongezea uwezo wakulima ikiwa ni pamoja na kuwafungulia viwanda vidogo na
vikubwa kwa ajili ya ubanguaji korosho.
No comments:
Post a Comment