02 September 2013

WASABATO MSITOE MICHANGO KANISANI KWA KUHUZUNIKA



Na Esther Macha, Mbeya
MBUNGE wa Rungwe Mashariki, mkoani Mbeya, Profesa David Mwakyusa, amewataka waumini wa Kanisa la Wasabato jijini humo, kuacha tabia ya kunung'unika wanapotoa michango inayokwenda kusaidia shughuli mbalimbali za kusaidia jamii
.Alisema baadhi ya waumini wamekuwa na moyo wa kujitolea wanapoombwa kufanya hivyo na makanisa yao kwani kazi ya Mungu ni kujitolea hivyo si busara kujutia ulichokitoa.
Prof. David Mwakyusa, aliyasema hayo hivi karibuni katika harambee ya ujenzi wa Kanisa la Wasabato, lililopo katika Kata ya Ntokela, Wilaya ya Rungwe, jijini humo.
"Ninachofahamu ni kwamba, muumini aliyeamua kujitoa ajitoe kwa nafsi yake mwenyewe si kwa shingo upande, naomba tubadilike kwani baadhi yetu wanaishi katika nyumba nzuri hivyo hivyo tunapaswa kujenga kanisa lililo bora," alisema.
Akisoma risala kwa mgeni rasmi, Mjumbe wa Kamati ya Maandalizi ya harambee hiyo, Bw. Awadi Mwandandila, alisema wameanzisha ujenzi wa kanisa hilo kutokana na wingi wa waumini ambao hivi sasa wanafikia 835.
Alisema ujenzi huo ulianza mwaka 2002 ambapo fedha zilizotumika hadi sasa ni sh. milioni 279 na zinazohitajika ili kukamilisha ujenzi huo ni sh. milioni 90.
Ka t i k a h a r amb e e h i y o , zilipatikana sh. milioni 46 ambapo zile zilizochangwa papo kwa papo sh. milioni 23, ahadi sh. milioni 23 na Prof. Mwakyusa na familia yake walichangia zaidi ya sh. milioni mbili.

No comments:

Post a Comment