02 September 2013

MIL.350/- KUTOLEWA MOTISHA WA WALIMU



 Na Rose Itono
SHULE ya Sekondari ya St.Matthew’s iliyoko Mk o a wa Pwa n i imetenga sh. milioni 350 kwa ajili ya motisha kwa walimu na wanafunzi watakaofanya vizuri kwa mwaka ujao katika mitihani yao ya mwisho ili kufanikisha mpango mkakati wa Matokeo Makubwa Sasa.

Akizungumza katika mahafali ya 13 ya kidato cha nne shuleni hapo mwishoni mwa wiki,Mkuu wa shule, Abrahamu Shafuri, alisema kuwa, baada ya serikali kuzindua mpango mkakati wa maendeleo unaoitwa Matokeo Makubwa Sasa, shule yake imeajipanga kuhakikisha inaboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia.
Alisema kwa mwaka huu shule ilitenga sh.milioni 306.6 kama motisha ya walimu,wanafunzi na wazazi kwani kufanya hivyo ni chachu ya mafanikio katika taaluma na kuamini kuwa kiasi hicho kitaleta ari na morali kwa watendaji ili kupata matokeo mazuri.
Alifafanua na kusema kuwa jumla ya sh. milioni 256 zitawezesha kuwasafirisha walimu nje ya nchi kwa ajili ya ziara za mafunzo ambapo pia wataweza kubadilishana uzoefu na kujifunza mbinu mbalimbali za kufundishia.
“Motisha za walimu na wanafunzi watakaofanya vizuri katika matokeo ya kidato cha sita shule imetenga sh.milioni 20.2, kidato cha nne, sh. milioni 16.1 na kidato cha pili sh.14,246,”,alisema.
Naye Mkurugenzi wa shule hiyo, Thadeus Mutembei, alisema ili kufanikiwa katika malengo hayo wadau wa elimu wanatakiwa kubadili mtazamo wa matokeo makubwa sasa kwa kujiuliza wanachangiaje matokeo haya.
“ I l i k u f a n i k i w a k a t i k a ma l e n g o y e t u tuliyojiwekea,tunahitaji wadau wetu wote kubadili mitazamo na kuwa na matazamo wa ‘Matokeo Makubwa Sasa,” alisema n a k u o n g e z a k u w a wadau hao ni pamoja na shule,wazazi,walimu na wanafunzi.
Mutembei alisisitiza kuwa wanafunzi wa shule hiyo kuongeza jitihada ili kujiandaa vyema na mtihani wa taifa kwa kuendelea kumtumainia Mungu siku zote, kushirikiana na walimu pamoja na wanafunzi

No comments:

Post a Comment