02 September 2013

WANANCHI WALIPWA FIDIA KUPISHA UCHIMBAJI SHABA



 Na Elizabeth Joseph, Mpwapwa
JUMLA ya wanakijiji 29 katika Kijiji cha Kinusi kilichopo Kata ya Ipera Wilaya ya Mpwapwa wamelipwa fidia kupisha uchimbaji wa madini katika eneo la Mlima Kitonge kijijini hapo.A k i z u n g u m z a k a t i k a makabidhiano hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya C.S.N inayojishughulisha na uchimbaji wa madini aina ya shaba katika eneo hilo, Juma Chibaya alisema jumla ya shilingi milioni 89 zimetolewa na kampuni hiyo kwa ajili ya kuwalipa fidia wanakijiji hao
.Chibaya alibainisha kuwa kitendo cha kuwalipa fidia wananchi hao ni moja kati ya makubaliano waliyopewa kuyafanya kabla ya kuanza shughuli ya uchimbaji huo ambapo kati ya hao 29, 22 ni wale waliokuwa na mashamba na saba ni waliokuwa na makaburi katika eneo hilo.Naye Mkurugenzi na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi katika kampuni hiyo, Cleopa Simule alisema kuwa mkataba wao katika eneo hilo ni miaka kumi ambapo tofauti na kuwalipa fidia wananchi hao pia kampuni yao inatakiwa kujihusisha katika shughuli nyingine za kijamii kijijini hapo ambapo hivi karibuni inatarajia kutoa madawati mia moja kwa ajili ya shule za msingi katika Kata hiyo.
"Mkataba wetu ni wa miaka kumi katika uchimbaji wa madini hayo hivyo katika kipindi hicho tumekubaliana pia kuhusika katika shughuli mbalimbali za kijamii na hivi karibuni tunatarajia kutoa madawati mia moja katika shule za msingi zilizopo katika kata hii ambapo awali tuliambiwa kuwa ndio changamoto kubwa inayowakabili walimu na wanafunzi katika kata hii," alisema Simule.Aidha alieleza kuwa bado kuna uelewa mdogo kwa wananchi juu ya sheria ya madini kwakuwa wengi wao wamekuwa wakikataa kulipwa fidia kwa madai kuwa hazilingani na madini yatakayopatikana katika maeneo wanayoyapisha.

No comments:

Post a Comment