Na Mwandishi Wetu
BENKI
ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma mpya itakayowapa nafasi wateja
binafsi wakubwa kupata huduma mbalimbali na kutimiza malengo yao.Kitengo cha
huduma hiyo iliyozinduliwa mwishoni mwa wiki kipo katika jengo la Coco Plaza,
jijini Dar es Salaam, na kitafahamika kama Kitengo cha Huduma Binafsi za
Kibenki kwa Wateja Wakubwa.
Akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi
huo, Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Dk. Reginald Mengi,
alisema huduma hiyo imekuja kipindi muhimu wakati Tanzania ikijizatiti
kiuchumi."Wakati nchi yetu ikikua kiuchumi,
mchango mkubwa sana unatolewa na taasisi za kibenki kama NBC. Idadi ya watu
wanaohitaji huduma za kifedha inaongezeka kila kukicha," alisema.
Alisema kwamba huduma hii ya kisasa ni
ya muhimu sana ikisisitiziwa na ukweli kuwa mashirika na makampuni
yaliyofanikiwa kibiashara ni yale yaliyofanikiwa kubadili mifumo ya kibiashara
kutokana na mazingira ya soka kwa manufaa ya wateja wao.
Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, mama
Mizinga Melu alisema kwa miaka 46 ya NBC nchini, benki hiyo imekuwa ikiendelea
kuongeza idadi ya wateja kutoka kila kada ya maisha wakiwa na mahitaji mapya na
tofauti.
"Ni kutokana na hilo ndio maana
tumeamua kuanzisha Huduma Binafsi za Kibenki kwa Wateja Wakubwa ambapo kitengo
chake kitakuwa kikitoa huduma kutokana na mahitaji maalumu," alisema.Mama Melu alisisitiza kwamba NBC
hufanya kila liwezekanalo kuwaandalia wateja wake mazingira bora ya kuhudumia
waweze kufikia malengo yao kirahisi.Ili mteja aweze kujiunga na Huduma Binafsi za Kibenki kwa Wateja Wakubwa
kutoka NBC atapaswa kuwa na kipato au mshahara usiopungua shilingi milioni 7.5
kwa mwezi..
No comments:
Post a Comment