Na Timothy Itembe,
Tarime
.WANANCHI
wa Kata ya Mriba Tarafa ya Ingwe wilayani Tarime mkoani Mara wamesema katiba
mpya ijayo itamke wazi haki za wanaume ili kuwalinda na unyanyasaji ambao
unafanywa na wanawake kwenye ndoa.
Wakitoa maoni
wananchi hao siku ya kukusanya maoni iliyoandaliwa na Chama cha Wakulima na
Wafugaji (CHAWAWATA) walisema kuwa kuna haja katiba ijayo itamke wazi haki za
wanaume asilimia 50 kwa 50 ili kuwalinda na unyanysaji ambao unafanywa na
wanawake wao wa ndoa.
Akizungumza
Diwani Mstaafu kata ya Mriba, Abdi Gasaya alisema kuwa baada ya wanawake kupewa
haki wametumia nafasi hiyo vibaya na kuwanyanyasa wanaume ikiwa ni pamoja na
kuwanyima tendo la ndoa kwa madai kuwa wamebakwa.
Mkazi wa Kijiji
cha Mangucha, Philipo Wambura alisema kuwa kutokana na wanawake kuwanyanyasa
wanaume kuna haja katiba ijayo itamke wazi haki za wanaume na kuwalinda dhidi
ya unyanyasaji uliopo kama vile kuwanyima chakula wakidai kuwa nenda ukale
uliko kuwa.
Aidha, wananchi hao waliongeza kusema
kuwa wanaunga mkono Tume ya Marekebisho ya Katiba ya Jaji Joseph Warioba
kupendekeza Tanzania kuwa na Serikali 3 Serikali ya Tanganyika, Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Pia waliongeza kusema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar na Serikali ya Tanganyika zitajitegemea kiuchumi aidha uchumi
utawezesha kila serikali kustawi bila kutegemea serikali nyingine
No comments:
Post a Comment