Na Queen
Lema, Arusha
ZAIDI ya wakulima
100,000 kutoka katika kanda mbalimbali nchini wamefanikiwa kupatiwa elimu ya
ufugaji wa ng'ombe ili kuongeza uzalishaji wao ambao sasa umeongezeka kwa zaidi
ya asilimia 80Wakulima hao
walipatiwa elimu hiyo ya ufugaji wa ng'ombe na kuku kwa kipindi cha miaka
miwili na Kampuni inayohusika na mifugo na mimea (KeenFeeders) iliyopo Jijini
hapa.
Hayo yalisemwa jana
na Ofisa Ugani wa Kampuni hiyo, Anzameni Muro, wakati akizungumza waandishi wa
habari kuhusu hali ya Kilimo Kwanza hasa kwa Mkoa wa Arusha na Kanda ya
Kaskazini kwa ujumla.
Muro alisema kuwa
asilimia kubwa ya wakulima na wafugaji nchini bado wanakabiliwa na changamoto
kubwa ya ukosefu wa elimu ndiyo maana kampuni hiyo ikaanza kutoa elimu hiyo.
Alisema baada ya
kuwapa elimu ambayo ilikuwa inahusu jinsi ya kupata faida kutokana na mifugo na
mimea wameweza kuongeza uzalishaji wa maziwa na nyama kwa kiwango cha asilimia
zaidi ya 80 tofauti na miaka iliyopita ambapo uzalishaji ulikuwa ni kama
asilimia 20 hadi 40.
"Ukiwa kama
mkulima au mfugaji ni lazima uweze kupata elimu, lakini hata vifaa ili kazi
unayoifanya isiwe ni kazi ya mazoea tu, kama wadau wa Kilimo kwanza tuliweza
kuliona hilo na tuliweza kuwapa elimu na kuwaelimisha hata namna ya kutumia
virutubisho kama vile madini aina ya ng'ombe Mix,"aliongeza Muro.
Muro alisema kupitia
elimu ya uhifadhi wa mazingira itaweza kuwasaidia wakulima wengi kwani mpaka
sasa takwimu zinaonesha kuwa wapo wakulima ambao wanalima wakijua wanahifadhi
mazingira, lakini kumbe
wanayahari
No comments:
Post a Comment