16 September 2013

SIMBA, MTIBWA ZAINGIZA MIL. 95/-



 Na Mwandishi Wetu
MECHI ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Mtibwa Sugar iliyochezwa juzi katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 95,080,000.Katika mechi hiyo, Simba ilitoka kifua mbele baada ya kuifunga Mtibwa mabao 2-0

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari na Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Boniface Wambura, watazamaji 16,507 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo.
Alisema viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 23,018,077.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 14,503,728.81.
Wambura alisema mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 11,704,107.18, tiketi sh. 2,548,890."Gharama za mechi sh. 7,022,464.31, Kamati ya Ligi sh. 7,022,464.31, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 3,511,232.15 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 2,730,958.34," alisema.

No comments:

Post a Comment