KIKUNDI
cha Waandishi wa Habari Wajasiriamali (Habari Group), kimepatiwa msaada wa
usafiri kwenda na kurudi mkoani Dodoma ili kujionea jinsi uendeshaji wa
shughuli za Bunge unavyofanyika, anaripoti Rachel Balama
.Msaada huo wa usafiri umetolewa na Bunge wa Jimbo
la Gairo,Ahmed Shabiby, ambapo mwaliko kwa kikundi hicho kwenda mkoani Dodoma
umetolewa na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angela Kairuki. Waziri huyo
ndiye mlezi wa kikundi hicho.Wa k i w a mk o a n i h umo wanachama wa kikundi
hicho watakuwa na mkutano na mlezi huyo pamoja na wadau
mbalimbali wakiwemo wabunge kwa ajili ya kusaidia
maendeleo ya kikundi.Akizungumzia udhamini huo, Shabiby alisema ameguswa
na malengo ya kikundi hicho, na kuamua kukisaidia kama mchango wake kwa
maendeleo ya taifa.Alisema, kwa kuwa kampuni yake ya usafirishaji
abiria ni ya kizalendo na huwa anatoa misaada kwa makundi mbalimbali kama hayo
kwa lengo la kuwakwamua kimaendeleo.
Mwenyekiti wa Habari Group, Mwanamkasi Jumbe,
alimshukuru kwa udhamini huo, ambao unahusisha usafiri na kwamba inawapa moyo
kuona viongozi na wafanyabiashara mbalimbali kuunga mkono juhudi za wasichana,
hasa wenye malengo ya kujikomboa.
Alisema waandishi wa habari wengi wamekuwa hawana
malengo, na mwisho wa siku kuishia pabaya, lakini wameamua kukusanya na kuweka
akiba zao kwa manufaa ya baadaye.Alimsifu Angela, ambaye amekuwa akijitolea kwa kiasi kikubwa kuhakikisha
kikundi hicho kinasonga mbele na kuomba wadau mbalimbali kujitokeza na kusaidia
makundi kama hayo.
No comments:
Post a Comment