02 September 2013

KIUNGO WA SIMBA AONGEZWA TAIFA STARS


  • WAWILI WAOMBEWA ITC UJERUMANI


Na Mwandishi Wetu
KIUNGO wa Simba, Jonas Mkude ameitwa kwenye kikosi cha Taifa Stars kinachojiandaa kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Gambia itakayochezwa Septemba 7, mwaka huu jijini Banjul.Kwa mujibu wa taarifa iliyolewa kwa vyombo vya habari jana na Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Boniface Wambura ilieleza kuwa Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen amemuongeza mchezaji huyo ili kuimarisha sehemu ya kiungo.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager, imeingia kambini tangu Agosti 29 mwaka huu kwenye Hoteli ya Accomondia jijini Dar es Salaam.Wambura alisema timu hiyo imefanya mazoezi jana asubuhi kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume wakati leo saa 10 jioni itafanya mazoezi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Katika hatua nyingine, Wambura alisema Chama cha Mpira wa Miguu cha Ujerumani (DBU) kimetuma maombi ya Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC), kwa wachezaji wawili wa Tanzania ili wajiunge na klabu mbili tofauti za nchini humo.
Alisema maombi hayo yaliyotumwa kwa TFF ni kwa ajili ya wachezaji Henry Claud Egito aliyezaliwa Desemba 31, 1984 jijini Dar es Salaam, na Dominic Johnson aliyezaliwa Agosti 14, 1991 jijini Tanga.
Wambura alisema achezaji hao wanaombewa ITC kama wachezaji wa ridhaa. Egito anaombewa hati hiyo ili ajiunge na Klabu ya FSV Lokomotive Dresden wakati Johnson anatakiwa na Klabu na TSV 1967 Schwabbruck

No comments:

Post a Comment