25 September 2013

MAAJABU YA MAITI DAR



  •  YAKUTWA NA DAWA ZA KULEVYA PIPI 33

 Na Frank Monyo

   Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limewashikilia watu wawili wakazi wa Tabata, kwa tuhuma za kukutwa na maiti ambayo tumboni ilikuwa na dawa za kulevya aina ya heroine.Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, Kamishna Suleiman Kova, aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari.


Alisema maiti hiyo ilikuwa na dawa hizo pipi 33 na kuwataja watuhumiwa kuwa ni Nasri Omari 'Roboti' (36) na Mwanaisha Salim (36), wote wakazi wa Kigogo Luhanga, wakiwa na mwili wa marehemu Rajabu Kadunda.

"Tulipata taarifa kuwa kuna mtu amefariki ghafla muda mfupi baada ya kutoka bafuni kuoga... tulikwenda eneo la tukio nyumbani kwa Omari na kuhoji hatimaye tuligundua uwepo wa maiti sebuleni ikiwa imelazwa chali katika godoro sakafuni.

"Omari ambaye ndiye mmiliki wa chumba kilichokutwa maiti, alisema marehemu ambaye kwa jina lingine anafahamika kama Mashaka Mabruki (43) ni mfanyabiashara," alisema.

   Aliongeza kuwa, uchunguzi unaonesha kuwa marehemu alifika Dar es Salaam akitokea mkoani Mtwara Septemba 21 mwaka huu, kwa maelezo kuwa ni mgonjwa na alikwenda kuchukuliwa na watuhumiwa hao ambapo muda mfupi kabla ya kifo chake, alikwenda bafuni kuoga na hatimaye kufariki dunia.

   Kamishna Kova aliongeza kuwa, mazingira ya kifo hicho yalisababisha polisi kufika eneo la tukio, kuchukua maiti na kuipeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi. "Uchunguzi uliofanywa na jopo la madaktari wawili pamoja na Maofisa wa Juu wa Polisi na ndugu wa karibu wa marehemu, zilikutwa pipi 33 za dawa za kulevya tumboni kwake.

"Pia marehemu alikutwa na hati ya dharura ya kusafiria nchi za nje ambazo hazikuonesha anasafiri kwenda nchi gani hivyo Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kubaini mtandao mzima wa usafirishaji dawa hizi uliomhusisha marehemu," alisema.

     Alisema zipo taarifa zinazoonesha marehemu alikuwa mhalifu mzoefu wa kusafirisha dawa hizo kwani kabla ya kurudi Tanzania alikuwa akitumikia kifungo nje ya nchi Barani Asia.Wakati huo huo, jeshi hilo l ime f a n i k iwa k umk ama t a Dismas Chacha (33), ambaye ni mfanyabiashara mkazi wa Tabata kwa kujifanya mtumishi wa umma (daktari).

      Kamishna Kova alisema, polisi walipata taarifa kutoka kwa raia mwema kuwa mtuhumiwa amekuwa akiwatapeli watu na kuchukua fedha zao akiwa na kawaida ya kuvaa mavazi ya kidaktari ambapo baada ya kupekuliwa, alikutwa na nyaraka mbalimbali zenye nembo ya Hospitali ya Muhimbili

No comments:

Post a Comment