05 September 2013

KIKWETE AONGOZA MAMIA MAZISHI YA ASKOFU KULOLA




 Askofu Kulola


 
Na Daud Magesa, Mwanza


RAIS Jakaya Kikwete jana amewa o n g o z a mami a y a waombolezaji katika mazishi ya Askofu Mkuu wa Kanisa la The Evangelical Assemblies Of God Tanzania (EAGT ) Moses Kulola.Mbali na Rais Kikwete mazishi hayo ambayo yalifanyika jana katika kanisa la Kalvary EAGT Bu g a n d o J i j i n i Mwa n z a , yalihudhuriwa na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, Mke wa Rais, Salma Kikwete,Katibu Mkuu wa Chadema, Dkt. Wilbroad Slaa na mkewe Josephine Mshumbusi, Katibu Mkuu wa ADC, Lucas Kadawi Limbu.


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Evarist Ndikilo, Wakuu wa wilaya mbalimbali,Wabunge wa CCM na Chadema wakiwemo, Maaskofu na wachungaji wa kanisa hilo.Akitoa salamu za rambirambi kwa wafiwa na waombolezaji waliohudhuria katika mazishi hayo, Rais alisema alipokea kwa masikitiko na majonzi makubwa kifo cha Marehemu Askofu Kulola.

Alisema marehemu alikuwa mtu mwema, muungwana ambaye alithamini sana watu na kuwapenda na hakuwa mtu wa kujikweza kama wanasiasa, bali alitumia muda mwingi kutumikia watu na hakuwa mbaguzi.

Rais alimwelezea Marehemu Askofu Kulola kuwa mahubiri yake yalihimiza upendo na kuhimiza watu kuishi bila kujali mahali walikotoka, rangi zao, makabila yao wala dini zao.

“Angekuwa hana sifa hizo asingekuwa rafiki yangu. Mimi si Msukuma, si Mkristo, wakati niko Ikulu alikuja kwangu na mama akaniambia amekuja kukuombea pamoja na nchi yetu kupitia kwako. Mungu atakuwezesha, kweli alikuwa mtu shupavu na mkweli,”alisema Rais Kikwete na kuongeza;

“Alikuwa mchungaji mwema wa kondoo wa Bwana na ni vigumu kuamini. Katangulia mbele ya haki nasi tutafuata kwa njia hiyo hiyo. Tumshukuru Mungu kwa kutupa fursa ya kuishi naye duniani kazi yake haina makosa.”

Aliwataka waombolezaji na waumini kuyaendeleza mazuri aliyoyasimamia na kuyadumisha mema a l i y o y a h u b i r i n a kuyaendeleza, tukiyafanya hayo hata machozi yetu yatakuwa na maana mbele za Mungu.

Awali katika Ibada ya mazishi iliyoendeshwa na Askofu Mkuu Msaidizi wa EAGT, Asumwisye Mwaisabila, alisema marehemu alikuwa mcha Mungu aliyejitolea kuwaleta watu kwa Yesu.Alisema na kuhoji atapatikana kijana gani wa kumuiga marehemu huyo kutokana na alivyojitoa kufanya kazi ya Mungu.

No comments:

Post a Comment