11 September 2013

KAMBI YA MAJAMBAZI 'YATEKWA'



Na Mwandishi Wetu
 Hali ya usalama katika kambi ya wakimbizi Ndutta,si nzuri kutokana na ongezeko la vitendo vya uhalifu vinavyofanywa na majambazi wanaofanya vitendo vya uhalifu nchunina wenzao kutoka nchi jirani ya Burundi. Kutokana na hali hiyo,Serikali ya Burundi imeitaka Serikali ya Tanzania kuendelea na msimamo wa kubadili matumizi ya ardhi katika kambi hiyo iliyopo wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma.

Akizingumza na Majira katika mahojiano maalum, Mkuu wa Wilaya hiyo, Bw. Venance Mwamotto,alisema Serikali ya Burundi imefurahishwa na msimahuo kwani majambaziwaliokuwa wakifanya uhalifu nchini kwao,walikuwa wakijificha eneo hilo.
“Kambi ya Nduta ipo mpakani mwa Tanzania na Burundi,baada ya wakimbizi waliokuwa wakiishi katika kambi hiyo kuondolewa, Serikali iliamua kugawa ardhi kwa vijana ili kuwa na kijiji cha mfano katika swala la kilimo.” alisema. Alisema awali Serikali ilitoa eneo hilo kwa vijana amabao badala ya kuayatumia kwa kilimo cha mazao ambayo yanayokubalika wao waliyatumia kwa kilimocha bangi,kuharibu mazingira na wengine kuchoma miti ili kupata mkaa na kuuza.
“Ni hali ya kusikitisha,tumeweza kubaini tatizo hili katika operesheni maalumtuliyoifanya katika eneo hili na kukamata kilo 1,500 za bangi” alisema Bw. Mwamottto. Alisema uamuzi wa kubadili matumizi ya ardhi hiyo ulifanywa na madiwani wa halmashauri hiyo na katika kikao cha maendeleo wilayani humo ambapo kilibariki azimio hilo. Kikao hicho pia kilihudhuriwa na mbunge wa Muhambwe,Felix Mkosamali
Aliongeza kuwa jambo la kushangaza Bw. Mkosamali watendaji wenzake na kuamua kufungua kesi mahakamani na kudai vijana wameny’ang’anywa ardhi. Bw. Mwamotto alisema kutokana na uhalifu uliokuwa ukifanyika eneo hilo umekuwa ulisababisha hofu kwa wananchi..
Alisema hivi sasa ,uongozi wa Wilaya hiyo na Jeshi la Polisi,umetangaza operesheni ya usalimishaji silaha,utoaji taarifa za siri kwa watu wanaojihusihsa na matukio ya uhalifu

No comments:

Post a Comment