Na Amina Athumani
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania
Bara Yanga, imeanza kukumbwa na majeruhi katika kikosi chake ambapo jumla ya
wachezaji watano jana walishindwa kufanya mazoezi kutokana na kuumia.Wachezaji hao
ni Simon Msuva, Kelvin Yondani, Mbuyu Twite, Ally Mustapha 'Barthez' na Mrisho
Ngassa
Akizungumza Dar
es Salaam jana, wakati wa mazoezi ya timu hiyo yanayofanyika katika shule ya
Loyola Mabibo,Dar es Salaam, Daktari wa timu hiyo Nasoro, Matuzya alisema
wachezaji hao kila mmoja anasumbuliwa na majeraha yake.Alisema kwa upande wa Twite ambaye
aliumia na kushonwa nyuzi tatu mdomoni, jana alijaribu kuingia mazoezini lakini
alishindwa kuendelea baada ya kupata maumivu makali kichwani .
Alisema Ngassa anasumbuliwa na kichwa
huku mchezaji Yondani bado akiwa na maumivu ya mguu aliyoyapata katika mechi ya
Ngao ya Jamii dhidi ya Azam FC na Msuva alipata majeruhi katika mazoezi ya
jana.
Alisema kutokana na hali zao mwalimu
hatawaingiza mazoezini hadi hapo watakapopata nafuu na kwamba wanategemea hadi
keshokutwa wachezaji hao watakuwa fiti kujiunga na wenzao kwa ajili ya
maandalizi ya mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.Katika pazia la Ligi Kuu Yanga wataanza kampeni zao za
kutetea taji hilo kwa kucheza na Ashanti United.
No comments:
Post a Comment