Na Amina Athumani
MSHAMBULIAJI mpya wa timu ya Simba,
Hamis Tambwe kutoka Vital 'O ya Burundi amewasili nchini jana kwa ajili ya
kujiunga na wekundu hao wa msimbazi.Akizungumza Dar es Salaam jana, Makamu
Mwenyekiti wa Simba, Joseph Itang'are alisema mchezaji huyo aliwasili jana kwa
ajili ya kuichezea timu hiyo katika msimu huu wa ligi kuu.
Alisema mara baada ya kuwasili tayari
Simba imeshakamilisha taratibu zote za mchezaji huyo kuichezea timu hiyo.Alisema mchezaji huyo ataondoka na
kwenda Kahama, Shinyanga kujiunga na kikosi cha timu hiyo kilichoweka kambi
ikiwa ni maandalizi ya kuelekea kuanza kwa mechi zake za ligi kuu.
Alisema wachezaji wote waliosajiliwa na
klabu yake watacheza katika ligi hiyo licha ya kuwepo kwa baadhi ya kasoro
katika usajili wao.Aliwataja wachezaji hao ambao usajili
wao ulikuwa na kasoro ndogondogo ni Betram Mombeki, ambaye amesema yupo tayari
kuichezea Simba kwa kuwa hakuna klabu iliyomuwekea pingamizi licha ya kuwepo
kwa taarifa zisizo rasmi za uwepo wa pingamizi.
Simba pamoja na klabu nyingine
13 za ligi kuu zipo katika maandalizi ya ligi hiyo ambayo itaanza kutimua vumbi
Jumamosi wiki hii. i.
No comments:
Post a Comment