Na Elizabeth Mayemba
MABINGWA wa Ligi Kuu Tanzania Bara,
Yanga jana wamekwaa kisiki baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Coastal
Union katika mechi ya Ligi Kuu iliyofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.Katika mechi ya
ufunguzi wa ligi hiyo, Yanga iliibuka na ushindi mnono wa mabao 5-1 dhidi ya
timu iliyopanda daraja msimu huu Ashanti United.
Mchezo ulianza
kwa timu hizo kusomana taratibu lakini, Coastal Union ilianza kufika lango la
Yanga ambapo dakika ya 17, Jerry Santo aliachia shuti kali akiwa nje ya 18
lakini mpira ukapaa juu ya lango.Dakika ya 23
lango la Yanga lilikuwa katika hekaheka tena baada ya Coastal Union kuliandama
lango la mabingwa hao ambapo, Yayo Litumba aliwatoka mabeki wa mabingwa hao na
kuachia shuti kali ambalo lilipanguliwa na Ally Mustafa 'Bathez' na kuwa kona
tasa.
Baada ya mashambulizi hayo, Yanga
iliamka na kuliandama lango ya Coastal Union ambapo dakika ya 35 Nadir Haroub
'Canavaro' alikosa bao la wazi baada ya kuachia shuti kali lililopaa juu ya
lango.Kipindi cha kwanza kilimalizika kwa
timu hizo kwenda mapumziko zikiwa hazijafungana, huku Coastal Union ikikosa
nafasi nyingi za kufunga.
Baada ya timu kurudi uwanjani kipindi
cha pili, Yanga ilicharuka na kufanikiwa kupata bao dakika ya 65 kupitia kwa
Didier Kavumbagu, baada ya kuunganisha krosi ya David Luhende.Dakika ya 75 mwamuzi wa mchezo huo,
Martin Saanya aliwatoa nje kwa kadi nyekundu wachezaji, Christine Odula na
Simon Msuva kwa kuchezeana rafu.
Wakati mashabiki waliohudhuria mechi
hiyo wakidhani mchezo huo ungemalizika kwa Yanga kutoka na ushindi, Coastal
ilipata bao la kusawazisha kupitia kwa Santo kwa mkwaju wa penalti baada ya
beki mmoja wa Yanga kuunawa mpira katika eneo la hatari.Katika mechi nyingine ya ligi hiyo,
iliyopigwa jana jijini Arusha katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Simba ilipata
ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji JKT Oljoro.
Simba katika mechi ya ufunguzi
ililazimishwa sare ya mabao 2-2 na Rhino Rangers ya Tabora ambayo imepanda
daraja msimu huu.Bao la Simba lilipatikana dakika ya 34
lililowekwa kimiani na Haroun Chanongo kwa shuti lililomshinda kipa wa JKT
Oljoro.
Hata hivyo dakika ya 50, Issa Kanduru
wa JKT Oljoro alikosa penalti baada ya beki wa Simba, George Owino kuunawa
mpira katika eneo la hatari akiwa katika harakati za kuokoa.Kutoka
Mbeya, Charles Mwakipesile anaripoti kuwa timu ya Mbeya City ilipata ushindi wa
mabao 2-1, dhidi ya JKT Ruvu katika mechi ya ligi hiyo iliyochezwa Uwanja wa
Sokoine.
No comments:
Post a Comment