29 August 2013

RAIS WBF ATOA NENO PAMBANO LA CHEKA



Na Fatuma Rashid
SHIRIKISHO la Kimataifa la Ngumi za Kulipwa (WBF), limeshukuru Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania TPBO kwa kufanikisha pambano la ngumi la kimataifa uzito wa kati.Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati wa kumtambulisha bondia Phil Wiliums kutoka marekani Rais wa WBF, Howard Goldberg alisema pambano hilo litasaidia kukuza mchezo wa ngumi hapa nchini
.Goldberg alisema katika mpambano huo kati ya Francis Cheka na Wiliums, mshindi atakwenda kupambana nchini Ujerumani Oktoba, mwaka huu na mbali na mpambano huo pia nchi ya Colombia imeomba pambano na Cheka.Alisema wameamua kuwapambanisha bondia, Thomas Mashali na Mada Maugo wote kutoka Tanzania ambao watawania ubingwa wa Dunia uzito wa kati, ili kuendeleza vipaji vya ngumi kwa mabondia ambao bado umri wao unaruhusu kuendelea na fani hiyo.
"Francis Cheka hivi sasa umri wake umeshakuwa mkubwa, hivyo tumeona ni bora kuzidi kukuza vipaji vya mabondia hawa wenye umri ambao bado ni mdogo, ili kukuza vipaji vyao na hapo baadaye wazidi kufanya vizuri," alisema.Naye bondia Wiliums, alisema amekuja kwa ajili ya kazi moja na atahakikisha anachukua mkanda huo, kwani anajiamini kuwa yeye ni bondia aneyefanya vizuri katika mchezo huo.
Kwa upande wake, Botha 'White Buffalo' alisema katika mpambano huo anatarajia kuona kitu cha pekee kutoka kwa mabondia hao, ili waweze kupata nafasi za kushiriki mapambano mengi zaidi."Mabondia hawa ninauhakika ni wazuri naamini wamejiandaa vizuri kwa ajili ya mpambano, hivyo kama wakifanya vizuri ninauhakika wataweza kushiriki mapambano mengi zaidi,"alisema.Naye mratibu wa pambano hilo, Jay Msangi alisema mpambano huo wa kimataifa ni wa kwanza kufanyika hapa nchini, hivyo itasaidia kuutangaza vizuri mchezo wa ngumi ndani na nje ya nchi.

No comments:

Post a Comment