29 August 2013

RIPOTI YABAINI UKATILI WA KUTISHA NCHINI



 Na Pendo Mtibuche, Dodoma
RIPOTI ya utafiti wa hali ya ukatili nchini kwa kipindi cha mwaka 2010 inaonyesha kuwa theluthi moja ya wanawake wote Tanzania wameathirika kwa namna moja au nyingne na ukatili wa kijinsia tangu wakiwa na umri wa miaka 15.Hali hiyo pia inaonyesha kuwa wanawake hao hao pia wameathirika na vitendo vya ukatili katika kipindi cha miezi 12 iliyopita.
Akizungumza na washiriki wa mafunzo y
a siku mbili kwa viongozi mbalimbali wa dini, Serikali na watumishi wa idara mbalimbali katika wilaya ya Bahi mkoani hapa juu ya mbinu za kuzuia ukali, Mwezeshaji wa mafunzo hayo kutosha Shirika la Women, Wake Up (WOWAP) chini la mradi wa tunaweza unaofadhiliwa na OXFAM Canada, Nasra Suleimani alibainisha hayo.
Alibainisha kuwa ukatili huo unaonekana kufanywa zaidi kwa wanawake waliotalikiwa, waliotengana na wenza wao au wajane.Nasra alisema kuwa takwimu zinaonyesha kuwa mwanamke mmoja kati ya watano amewahi kufanyiwa ukatili wa kingono huku asilimia kumi ya wanawake inaonyesha walifanya mapenzi kwa kulazimishwa yaani bila idhini yao.
Al i s ema k uwa l e n g o l a kuanzishwa kwa mradi huo wa tunaweza ni kuweza kupunguza hali ya watu kukubali ukatili na kuona kwamba ni jambo la kawaida kumfanyia mwanamke vitendo ambavyo kimsingi ni ukatili.Aidha alisema kwamba kampeni hiyo itawezekana kwa kujenga umma unaopinga ukatili dhidi ya wanawake dhidi ya ya ukatili na kushawishi jamii uacha vitendo hivyo.
Hata hivyo, alisema kuwa vitendo hivyo vinaonekana kushamiri kutokana na kuwepo kwa tabia ya baadhi ya watu kuwa na mtazamo wa jamii kuwa ni halali mwanamke kupigwa.Vilevile alisema kuwa tatizo lingine la kuendelea kuenea kwa ukatili kunatokana na wanawake wenyewe kuona ni haki kupigwa wanapokuwa wamefanya kosa.
Alisema kuwa wao kama wao wanajitahi kutoa elimu kwa jamii kwa kuwaelimisha wananchi kutumia mbinu mbalimbali ili waepukane na ukatili huo.Miongoni mwa mbinu hizo ni pamoja na kuhamasisha mtu mmoja mmoja kubadili tabia zao juu ya ukatili na kujenga washirika, kujenga muonekano wa kampeni kupitia mbinu mbalimbali

No comments:

Post a Comment