05 August 2013

WAZIRI MAKALA AZIPA SOMO TAASISI ZA FEDHA NCHINI


 Na Mwandishi Wetu
TAASISI za fedha nchini zimeshauriwa kutoa mikopo yenye masharti nafuu kwa taasisi za elimu ili ziweze kujipanua na kuchangia kuinua kiwango cha elimu nchini.Ushauri huo ulitolewa mwishoni mwa wiki na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Amos Makala, wakati akizungumza kwenye mahafali ya Shule ya Fountain Gate, Tabata jijini Dar es Salaam, kukiwa na wahitimu 74 wakiwemo wa darasa la saba na chekechea.

Alisema hakuna haja kwa taasisi hizo kuogopa kuzikopesha taasisi za elimu kama Fountain Gate kwani zina mali nyingi zisizo hamishika zinazoweza kutumika kama dhamana."Benki zikiwakopesha wataweza kujipanua zaidi na Watanzania wengi watapata fursa ya kusoma na katika elimu humo watapatikana akina Kikwete (Rais Jakaya Kikwete), Pinda (Waziri Mkuu Mizengo Pinda) na wengine, nashauri taasisi za fedha ziwe karinu na wadau wa elimu," alisema.
Awali, Mkurugenzi wa shule ya Fountain Gate, Japhet Makau, alisema taasisi za fedha nchini zimekuwa na urasimu mkubwa katika utoaji wa mikopo kwa taasisi za elimu hapa nchini.
Alisema taasisi za fedha zinapaswa kuachana na urasimu huo na kuzipatia mikopo yenye masharti nafuu taasisi za elimu ili ziendelee kutoa mchango mzuri katika kukuza elimu.
Makau alisema taasisi za fedha zinatakiwa kuwa na mwenendo wa kibiashara wa taasisi za elimu na kubuni huduma zinazoendana nazo.
Katika hatua nyingine, alisema shule hiyo imeanzisha utaratibu wa kuwafadhili watoto yatima kusoma katika shule hiyo kila mwaka ili wapate elimu bora kama wenzao wenye wazazi.
Alisema mwaka jana shule hiyo iliwafadhili kwa asilimia 100 wanafunzi wawili kwa kuwalipia ada, mavazi, gharama za hosteli na vifaa vingine vinavyohitajika.
"Fountain Gate tangu kuanzishwa kwake imekuwa ikijali na kuwakumbuka watoto ambao wameshindwa kupata fursa ya elimu baada ya kupoteza wazazi wao, familia ya shule hii wakiwemo wazazi, wafanyakazi na wanafunzi wamekuwa wakiwasaidia nguo, vyakula na vifaa vya usafi," alisema.
Alisema Fountain Gate inajitahidi kutoa elimu kamili kwa kutoa elimu kwa watoto wakiwa bado wadogo hadi chini ya miaka miwili, kucheza, kujifunza kupitia michezo na kutoa msukumo wa kujifunza kupitia ziara za mafunzo

No comments:

Post a Comment