05 August 2013

WAHIMIZWA KUTHAMINI BIDHAA ZA NDANI


 Na Pendo Mtibuche, Dodoma
TANZANIA inakabiliwa na tatizo la watu kutopenda bidhaa zinazozalishwa nchini na badala yake kukimbilia kuchangamkia zile bidhaa zinazotoka nchi za nje.Hayo yalielezwa jana na Mkurugenzi wa Veta Kanda ya Kati, Fredrick Mushi, wakati akizungumza na gazeti hili katika viwanja vya Maonesho ya Wakulima na Wafugaji Nane Nene Nzuguni mjini hapa.

Kutokana na hali hiyo, mkurugenzi huyo alisema VETA imekuwa mstari wa mbele kuwasogezea huduma wananchi na kuwapatia elimu, hasa katika maonesho hayo ya wakulima ili waweze kuona ubora wa bidhaa mbalimbali zinazozalishwa hapa nchini.
Al i s ema k uwa b i d h a a zinazozalishwa nchini zikiwemo zile zinaozalishwa na VETA ni bora na hazina madhara kwa mlaji au mtumiaji, hivyo Watanzania hawana sababu ya kukimbilia bidhaa za nje na badala yake wajenge utamaduni wa kutumia bidhaa za ndani.
Hata hivyo, alisema kuwa bidhaa mbalimbali ambazo wanazalisha ni zile zinazotokana na mbao, mazao ya chakula, mboga mboga na zote hizo zinalenga kumuelimisha mkulima ili aweze kuona ni jinsi gani watapenda bidhaa za ndani.
Akizungumzia maonesho hayo, alisema kuwa VETA imejikita kutoa elimu kwa jamii kuhusiana na mafunzo yanayotolewa katika vyuo vyao vilivyopo kanda ya kati.
Alisema endapo bidhaa zinazozalishwa zinakuwa chini ya kiwango walaji au watumiaji ndiyo wenye uamuzi wa mwisho wa kutozitumia bidhaa za aina hiyo ili kutoa fursa kwa mtengenezaji aweze kuziboresha.

No comments:

Post a Comment