Na Rachel Balama
WATUMISHI wa
Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) wametakiwa kuongeza juhudi, umoja na maarifa
ili kuhakikisha wanafanya kampuni hiyo inakuwa ya mfano wa kuigwa ndani na nje
ya nchi.Ushauri huo
ulitolewa na aliyekua Mwanasheria Mkuu wa Kampuni wa TTCL, Gilder Kibola,
wakati akizungumza na wafanyakazi na menejimenti ya kampuni hiyo kwenye hafla
ya kumuaga mwishoni mwa wiki Dar es Salaam.
Alisema ni
muhimu kwa wenzake wanaobaki kuendeleza juhudi na kumpa ushirikiano Ofisa Mtendaji
Mkuu wa kampuni hiyo ili aweze kufikia malengo yake.
"Nawashauri muendelee kumpa
ushirikiano kiongozi wetu ili malengo yake aweze kufikiwa," alisema.
Kibola alisema kufanikisha mipango na malengo ya kampuni hutegemea ushirikiano
na mshikamano katika utekelezaji wa majukumu yake.Kibola alijiunga na kampuni hiyo mwaka
1996 akiwa kama Afisa Sheria na kupanda ngazi hadi kufikia nafasi hiyo ambayo
amestaafu nayo.
" N i n a s h u k u r u Mu n g u
namaliza salama na afya njema, nimejifunza mengi naomba vijana katika kampuni
hii kuhakikisha mnajifunza kwa waliowatangulia utendaji kazi mzuri kwa
kuzingatia busara na weledi," alisema" J i f u n z e n i k w a w a t u wa
l i owa t a n g u l i a k a z i n i , mtafanikiwa," alisema.Ofisa Mkuu Mtendaji wa TTCL, Dkt.
Kamugisha Kamuzora, alisema kampuni itamkumbuka kwa mchango wake wa uchapaji
kazi.
Mkuu wa utumishi wa Kampuni hiyo, Juvenal
Utafu alisema, Kibola amekuwa pamoja na kampuni katika vipindi mbalimbali
vilivyopitiwa na TTCL na hakutetereka hadi anastaafu kwa heshima.Aliongeza kwamba alikuwa kiungo muhimu kati ya
wafanyakazi na bodi na amechangia mafanikio katika idara ya sheria.
No comments:
Post a Comment