13 August 2013

WAZAZI WAHIMIZWA KUSHIRIKIANA NA WALIMU KUONGEZA UFAULU



 Na Penina Malundo
WA Z A Z I n a w a l e z i n c h i n i w ame s h a u r i w a kufuatilia kikamilifu maendeleo ya kitaaluma ya watoto ili kupunguza ongezeko la matokeo mabaya ya mitihani yao ya mwisho.Ushauri huo ulitolewa hivi karibuni jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Jimbo la Kati la Dayosisi ya Mashariki (KKKT), Chediel Lwiza wakati wa mahafali ya tatu ya wahitimu wa Shule ya Msingi ya Mount Zion iliyopo jijini humo
. Lwiza alisema kuwa kutokana na wimbi kubwa la ongezeko la wanafunzi wanaofeli kidato cha pili na nne ,ipo haja ya wazazi na walezi kushirikiana na walimu, kuhahikisha wanaimarisha misingi ya elimu kuanzia nyumbani wanapotoka watoto hadi wafikapo shuleni.
"Elimu bora inatokana na ushirikiano mzuri baina ya mwalimu na mzazi na hapo mzazi unauwezo wa kupokea matokeo mazuri kutoka kwa mtoto kwani jukumu la kusimamia kama mtoto anasoma si la mwalimu peke yake bali hata mzazi anawajibu wa kusimamia mwenendo wa masomo ya mtoto wake hasa kipindi mtoto yupo nyumbani," alisema Lwiza
Alisema asilimia kubwa ya jamii inayowekeza katika elimu inauwezo mkubwa wa kutengeneza Taifa lenye maendeleo na lenye kuleta misingi imara itakayoweza kuleta tija ya kuinua nchi katika nyanja ya uchumi, kijamii na kisiasa.
Aidha alisema kuwa shule za msingi pamoja na sekondari zinatakiwa kuwafundisha wanafunzi kwa njia ya vitendo zaidi hasa somo la ujasiriamali kama somo la ziada litakalomuwezesha mwanafunzi pindi atakapo maliza shule na kukosa ajira kuweza kujiajiri mwenyewe.
"Hakuna mtoto hata mmoja anayezaliwa akawa mbumbumbu, ila Mungu kila mtu kampatia uwezo wake hivyo nashangazwa na Wazazi wanaokata tamaa dhidi ya watoto wanaofeli mitihani kwani mungu anajua kuwa kila mtu anauwezo wa kufanya jambo fulani, hivyo ni vyema tukawekeza watoto wetu elimu iliyobora nakuimarisha misingi imara ya elimu itakayomfanya watoto waondokane na kufeli," alisema.
Jumla ya wanafunzi 29 wa Shule ya Msingi Mount Zion waliomaliza darasa la saba na awali, wamekabidhiwa vyeti vyao katika mahafali hayo.

No comments:

Post a Comment