Na Yusuph
Mussa, Lushoto
MK U U w a Wi l a y a y a Lu s h o t o ,
Al h a j j M a j i d M w a n g a amesema ataendelea kuwashughulikia watendaji
wa kata na vijiji wanaodharau utawala wake kwa kusema kwa sasa Jimbo la Bumbuli
halina Mkuu wa Wilaya hivyo kukataa kutii maagizo yake.
Akizungumza
juzi kwenye warsha ya siku mbili kwa watendaji wa vijiji na kata wa Halmashauri
mpya ya Bumbuli ili kufundishwa majukumu yao,
aliwaasa watendaji hao kuwa pamoja na Bumbuli kupata halmashauri mpya, bado ipo
chini ya Mkuu wa Wilaya ya Lushoto.
"Kuna
watendaji wa kata kama wanne hivi nimesikia wanasema baada ya kupata
halmashauri sasa wanasubiri Mkuu wa Wilaya yao na kudharau maagizo yangu. Nasema
watendaji hao wanajidanganya kilichopatikana ni halmashauri, lakini Mkuu wa
Wilaya bado ni mmoja.
"Na hilo
si ajabu, Moshi kuna Manispaa na Halmashauri ya Moshi Vijijini, na Arumeru ni
vivyo hivyo. Si mnasema mimi ni mzee wa kuweka watendaji ndani, basi endeleeni
kusema mimi si Mkuu wa Wilaya ya Halmashauri ya Bumbuli, lakini mtakiona kile
ninachosema," alisema Mwanga.
Mwanga alisema kata nyingi ofisi zao
zinafungwa muda wa kazi, huku baadhi ya watendaji wanaondoka maeneo ya kazi na
kuwaachia watoto na ndugu zao kukaimu matokeo yake siri za Serikali zinakutwa
zimesambaa mitaani.
"Itabidi tuwaite mashekhe na
wachungaji wawaombee watendaji hawa kwa kushindwa kuwajibika. Nilitumia usafiri
wa binafsi na kukuta kata nane zimefungwa na watendaji hawapo kazini, sijui
tutafute shekhe na mchungaji awaombee viongozi hawa.
"Lakini wamekuwa na tabia ya
kuondoka eneo la kazi na kuwaachia ofisi watoto na ndugu zao wanakaimu, kesho
yake utakuta nyaraka za siri za Serikali zipo mitaani. Lakini utakuta vikao
havifanyiki, lakini wanaghushi mihutasari kuonesha kuna watu wamehudhuria, tena
kikao hicho utakuta ni cha kutoa fedha," alisema Mwanga.
Mwanga alisema anafahamu kuwa baadhi ya
watendaji wanakaimu zaidi ya miezi kumi bila kulipwa mshahara wala posho,
lakini hicho kisiwe kigezo cha kuwafanya kucheza mchezo mchafu na kuiba fedha
za miradi ya wananchi inayopelekwa kwenye kata na vijiji vyao na kuamini
halmashauri italipatia ufumbuzi tatizo hilo.
Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri ya Bumbuli, Beatrice Mshomisi alisema maudhui ya warsha hiyo ni
kuwakutanisha watendaji hao ili waelewe majukumu yao, lakini pia waeleze
changamoto wanazokutana nazo sehemu za kazi.
Hivi karibuni Ofisa Mtendaji wa Kata ya Vuga,
Ali Shenkawa aliwekwa ndani na Mkuu wa Wilaya baada ya kudaiwa kupuuza agizo la
kuwaeleza viongozi wa vijiji ambao ni Mwenyekiti na Mtendaji kila kijiji
washiriki kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama cha Tarafa.
No comments:
Post a Comment