12 August 2013

WATU WENYE MATATIZO YA MOYO WAPEWA USHAURI



 WATU wenye matatizo na maradhi ya moyo wametakiwa kutotumia kinywaji kipya cha Chilly Willy ili kujiepusha na usumbufu ambao ungeweza kuwapata kama wangetumia kinywaji hicho pasipo kujua madhara yake, anaripoti Mwandishi Wetu.

Ushauri huo umetolewa na Meneja Uhusiano wa Super Market ya TSN, Meshack Nzowah, wakati wa promosheni ya kinywaji hicho iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Akizungumza katika hafla hiyo Nzowah alisema Chilly Willy ni kinywaji kisicho na kilevi kinatumika kwa watu mbalimbali na kinaongeza nguvu kwa watumiaji, lakini kwa watu wenye matatizo ya moyo hakiwafai.
Aliongeza kuwa kinywaji hicho kinachotengenezwa Dubai, kinapendwa na watu mbalimbali duniani hususan wanamichezo na kimekuwa kikiwaongezea nguvu.
“Baada ya kuona kinywaji cha Chilly Willy kinatumiwa na watu wengi duniani, tumeamua kukileta Tanzania ili watu waanze kukitumia kwa kweli ni kinywaji bora na kinakata uchovu wa pombe,”alisema Nzowah.
Watu wengine ambao hawatakiwi kutumia kinywaji hicho ni watoto walio chini ya miaka 10. Aliwataka Watanzania waanze kutumia kinywaji hicho.
Licha ya uzinduzi huo kufanyika jijini Dar es Salaam, pia uzinduzi kama hao ulifanyika visiwani Zanzibar ambapo wananchi mbalimbali wameshauriwa kutumia kinywaji hicho.

No comments:

Post a Comment