05 August 2013

WATENDAJI WATAKIWA KUWA WABUNIFU KUBORESHA MIPANGO MIJI


Na Hamisi Nasiri, Masasi
MBUNGE wa Jimbo la Masasi (CCM)mkoani Mtwara, Mariam Kasembe amewataka watendaji katika Halmashauri ya mji wa Masasi kuwa wabunifu katika suala la mipango miji ili kuufanya mji huo uwe katika mandhari ya kuvutia hatimaye kuondokana na tatizo la ujenzi holela.

Mbunge huyo aliyasema hayo mwishoni mwa wiki kwenye kikao cha kawaida cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya mji wa Masasi wakati alipokuwa akitoa nasaha kwa madiwani na watendaji wa Halmashauri hiyo, baraza hilo lilifanyika katika ukumbi wa nje wa karakana ya maji mjini hapa.
Alisema kuwa watendaji waliopo kwenye Halmashauri hiyo ni lazima wawe wabunifu katika kuhakikisha kuwa mji huo unakuwa safi na kuhakikisha kuwa wananchi wanajenga majengo yao kuendana na kanuni na taratibu za mipango mji zinavyotaka ili mandhari ya mji iwe katika hali inayotakiwa.
Kasembe alisema kuwepo kwa tatizo la mipango mji katika mji wa Masasi linaweza kwisha iwapo kila mtendaji kwa nafasi yake atakuwa mbunifu katika kutimiza wajibu anaotakiwa kuufanya hatimaye mji kuwa kwenye mwonekano unaotakiwa na hata ubunifu huo pia utasaidia kuleta maendeleo mengine kwa wananchi.
Alisema kuwa msingi wa mji kuwa katika mandhari inayotakiwa kutokana na watendaji husika kuwa wabunifu kwenye kubuni na kusimamia mipango mbalimbali ya kuuweka mji kwenye ramani mzuri ya kuvutia na kufanya tatizo la makazi holela kutoweka.
Ai d h a mb u n g e h u y o a l iwa s h a u r i wa t e n d a j i waliyopo kwenye Halmashauri hiyo kuhakikisha kuwa wanatekeleza ipasavyo mahitaji yanayowagusa wananchi ili kupunguza malalamiko yasiyo na msingi ikiwemo malalamiko ya viwanja ambapo katika eneo la kata ya Nyasa na Mtandi baadhi ya wananchi wamelipia zoezi la upimaji lakini hadi sasa upimaji haujafanyika.
"Nawaomba watendaji kuweni wabunifu ili mji wetu uwe katika mandhari ya kuvutia kwa wageni wanaoingia na kutoka lakini kama msipokuwa na ubunifu mji utaendelea kuwa katika hali mbaya ...pia naomba kila mtendaji kupitia nafasi yake pia awe mbunifu ili kwa pamoja tuweze kuwatimizia wananchi kile wanachokihitaji," alisema mbunge huyo.

No comments:

Post a Comment