Na Heri Shaaban
WAFANYAKAZI wa
Shirika la Reli la Tanzania na Zamb i a (TAZARA) wamepanga kuandamana kwenda
Ofisi za Waziri Mkuu Mizengo Pinda kufikisha kilio chao baada ya kufanya kazi
kwa muda wa miezi mitatu bila kulipwa mishahara yao
.Hatua ya
kupanga maandamano ya kwenda kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda kupeleka kilio chao
inafuatia mawaziri karibu wanne waliokaa katika Wizara ya Uchukuzi akiwemo
Harrison Mwakyembe kushindwa kuyapatia ufumbuzi matatizo ya wafanyakazi wa
TAZARA na Uongozi.
Akizungumza na
waandishi wa habari, Dar es Salaam jana, Katibu wa Wafanyakazi Kanda ya Dar es
Salaam TAZARA na TRL (TRAWU) Erias Chizingwa alisema kesho Jumatatu watakutana
katika kikao cha TRAWU baada ya kikao cha mwishoni mwa wiki kushindwa kutoa
majibu.
Chizigwa
alisema wamepanga kukutana Agosti 5, mwaka huu katika kikao chao ili kutoa
maamuzi ya kupeleka kilio chao kwa Mizengo Pinda ili aweze kushughulikia
malalamiko yao ya kucheleweshewa mishahara toka mwezi Mei hadi sasa.
"Mimi sio
msemaji lakini, tunataka kufanya maamuzi hayo katika kikao chetu cha pamoja
wafanyakazi wote wa TAZARA kwenda kwa Pinda au aje kusikiliza kilio chetu na
kutolea ufumbuzi baada ya mawaziri zaidi ya wanne waliokuwepo awali na sasa
hivi, katika Wizara ya Uchukuzi kushindwa kushughulikia matatizo ya mishahara
na changamoto zinazotukabili kama wafanyakazi.
Alisikitishwa
na Jeshi la Polisi kuingilia kuvuruga mkutano wao wa Agosti 2, mwaka huu pamoja
na kupora kamera ya mwandishi wa Kituo cha Chanel Ten Elia Ruzika na kumfunga
pingu, wakidai mkutano huo sio halali ulioandaliwa na Chama cha Wafanyakazi wa
Njia ya Reli TRAWU wakati ulifuata taratibu zote na kupewa kibali.
Wa k a t i h u
o h u o , Ka t i b u wa Shirikisho la Vyama Vya Wafanyakazi nchini (TUCTA) Mkoa
wa Dar es Salaam, Mussa Mwakalinga amelionya Jeshi la Polisi kuacha kuingilia
kati kinyume cha taratibu ya mafunzo yao.
Mwakalinga ametoa tamko hilo
kutokana na kusikitishwa na mwenendo wa kazi wanazofanya Jeshi la Polisi kuvuruga
mikutano ya wafanyakazi wakati wakidai maslahi kazini ili waweze kupata haki
zao.
"Jeshi la Polisi kazi yake ni
kulinda usalama wa raia na mali zao sio kuvuruga mikutano au kupiga raia wakati
wakidai haki kama walivyopora vifaa vya mwandishi wa Chanel Ten na kumfunga
pingu, kwani kila mtu ana uhuru wa kutumia na kutoa mawazo yao hadharani kama
katiba inavyoruhusu,"alisema Mwakalinga.
Alisema utaratibu waliotumia
wafanyakazi TAZARA ni mzuri wa kuomba kibali na kukutana, sio kama wafanyakazi
wa nchi za wenzetu wanatumia nafasi yakupeleka kilio chao kwa maandamano
barabarani.
Alisema kama polisi wanatumwa na
Serikali alishauri polisi wajiunge na vyama vya wafanyakazi waweze kufundishwa
sheria za kazi kwa ajili ya kulinda, kutetea na kudumisha mauhusiano ya kazi.
Mungu walaani wote waliochagia TAZARA kushindwa kujiendesha kifaida ni mafisadi hao Mungu waangamize jehanamu wakimaliza maisha yao hapa duniani amina
ReplyDelete